Sikiliza mkuu, toka enzi na enzi wazee wetu walikuwa wanalea watoto wasio wao, na walikuwa wanajua kabisa huyu damu yangu, huyu si damu yangu.
Kiutaratibu ni kwamba watoto wote watakaozaliwa ndani ya ndoa ni wako no matter what. Hata mke akikimbia kwako, akienda kuzaa huko aliko wazee wetu walikuwa wanaenda kuwabeba hao watoto. Yani as long as umemlipia mahari basi watoto wote atakaozaa ni wako..
Shida ya kizazi cha sasa hatujui wazee wetu waliishi vipi enzi hizo mpaka wakaweza ku maintain social order✅. Sisi tunahisi haya mambo ni mapya, lakini yapo enzi na enzi.
Huyo mtoto wako na ataendelea kuwa wako no matter what, mkeo kuropoka ni jambo moja na mtoto kutokuwa wako ni jambo jingine kabisaaa, tena ameshakuwa mkubwa 10yrs?
Wewe relax, endelea na maisha yako, mwanaume hupaswi kuwa na stress na vitu vidogo kama hivi, huo ndiyo uanaume mkuu..