Mke bora na mwema

Mke bora na mwema

EricMan

JF-Expert Member
Joined
Oct 5, 2017
Posts
3,701
Reaction score
6,441
Mke mmoja aliulizwa:

Ni kipi kimemfanya mumeo akupende kiasi kwamba asione yeyote mwengine duniani wa kumsifia ila wewe, Ilhali wapo wenye uzuri kukuliko?

Akajibu

Hakika sikuwa mzuri wala sina uzuri wa kumfanya awe hivyo unavyosema.

Ninachofahamu ni kuwa:

Nimuonapo mume wangu anakuja au aniangaliapo usoni hutabasamu na kukunjua sura yangu.

Anapokuwa na jambo humsikiliza kwa umakini na huacha yote nimtekelezee aloniagiza ingawa nilikuwa na ya muhimu mengine.

Anaponipatia kingi au anileteapo zawadi humsifia na kuisifu zawadi hiyo hata ikiwa sio katika ninavyovipenda.

Anapokosa kikubwa akaniletea zawadi ndogo mfano wa pipi hutosheka na humuombea apate mengi na makubwa zaidi.

Humfanya yeye ndiye wa kwanza nyumbani kabla ya watoto na wengine wote.

Simkati neno hata kama sipendi kulisikia
 
Wapo lakini wamepungua sana, tofauti ya wanawake wa Zamani na sasa ni kuwa wanawake wengi wa Zamani waliona fahari kuolewa na wengi walikuwa hawajishughulishi sana na ajira hivyo mme ndiyo ilikuwa kila kitu Hali hii ilisaidia sana kuwafanya kina mama kuwa waminifu na watii, hata sasa Kuna baadhi ya nchi kama China na maeneo ya nchi za kiarabu kwa kuwa mifumo Yao siyo ya Haki Sawa kama kwetu wanawake wa kule bado Wana tabia na utiii kama wa kwetu wa Zamani, hivyo inanyesha madhara ya mwanamke kumpa uhuru afanye awezavyo hili halipingiki
 
Wanawake hao sasa hivi wamekuwa bidhaa adimu sana!kuwapata inachukua karne!
 
Back
Top Bottom