Mitihani ya maisha

jong 255

Member
Joined
Jul 31, 2017
Posts
98
Reaction score
49
Nimetengwa na ndugu na marafiki apo zamani nilikuwa namarafiki wengi na ndugu pia walinipenda.
Ila cha ajabu saiz naweza kusema sina marafiki kabisa baadhi ya ndugu pia wamenitenga ninachekwa kwa mambo yauongo nadhalauliwa kilamtu ananiongelea vibaya kwa maneno tu yakuskia kwa watu

Nashukuru mungu kuna baadhi ya watu tunaheshimiana na kunabaadhi ya ndugu pia wanipenda

Mwenyezi mungu naomba aendelee kunipa nguvu nipambane na maisha yangu sitaki kumwangalia mtu anijalie katika njia zangu za maisha.

Naamini ipo siku wote wanaonicheka,kunidhalau,kunidhalilisha na kunisimanga watabaki vinywa wazi.

Nimeathilika kisaikolojia siwezi kumuamini mtu naona kama wote in walewale.

Ninachoamini duniani tunapita namuomba mungu azidi kunijalia niishi vyema mpaka atakapo nichukua...

Asanteni na usiku mwema..mungu awabariki.
 
Raha jipe mwenyewe
Toka kafurahi kwa raha zako.
Hakuna atakae kufurahisha ila mwenyewe
 
Ukiwa na pesa mingi utapendwa tu hahaaa utaitwa sweet mangi ama sweety manka
 
Hii Hali ilishawahi kunipata nikabakia na watu wawili tu walioweza kunipa moyo bibi na dada yangu ila nashukuru Mungu niliivuka.

Hii hali kila mmoja anaweza akaipitia ila kuvuka salama ni wachache maana unaweza hata ukajiua.
 
Ni hisia tu ulizonazo, ni hali tu ya kisaikolojia ambayo umhijia mtu hasa mambo yaendapo ndivyo sivyo. Mara nyingi inakuja kwa wale wanaodhani watu wanawapenda kwasababu wana hela, wana uwezo! Kumbe upendo kwa mwanadamu inakuja automatic, it's inborn! We we wapende tu, ukijizuia ni kama kuondoa uchafu kwa kutumia uchafu! Saikolojia ni nzuri sana! Ikiijua!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…