Ni wazi kutokana na kujitokeza hali tete yenye mivutano na kutoelewana miongoni mwa Wanasiasa wa juu ndani ya Chadema, kushutumiana, kulaumiana, kutengana na kutupiana maneno makali wenyewe kwa wenyewe ni kama mfano wa Manahodha wanaogombania usukani huku wakiwa katikati ya kina kirefu cha Bahari.
Hivi sasa hakuna tena siri ya kuficha jambo hilo au hitilafu zilizopo kutokana na viongozi wake muhimu kugawanyika hali iliyowasukuma hata Wanachama nao kila mmoja kuchagua na kufuata kundi au upande anaouona una manufaa kisiasa kwake .
Upo ushahidi wa moja kwa moja usemao Waziri Mkuu aliyejiuzulu kwa Kashfa ya Richmond Edward Lowassa, amerudia tena indhar yake akiwataka viongizi wenzake wa Chadema kujibadili toka kwenye kundi la uanaharakati ili kujigeuza na kuonekana ni kikosi adili cha Wanasiasa.
Kwa mara ya kwanza Lowassa alipotoa matamshi hayo alizusha tashwish na maneno mengi ndani ya Chadema huku baadhi ya viongozi hadi kufikia kumwambia yeye si mwalimu wa siasa wa kuifundisha Chadema na viongozi wake hivyo akubaliane na utamaduni wa Chama hicho au arudi CCM.
Lowassa akaonywa akitakiwa asijifanye Mwalimu Julius Nyerere ndani ya Chadema. Lowassa akubali na ashukuru kukaribishwa, kupewa nafasi ya kuwania urais mwaka 2015 ila akitakiwa awaachie chama chao kama alivyokikuta.
Madai ya Lowassa yanawataka wenzake wajitahidi kukiweka chama hicho katika mikono salama ya kuheshimika mbele ya Jumuiya za Kimataifa, Mashirika ya kidunia pia kiweze kuzivutia nchi wahisani, viongozi wa madhehebu za dini kwa kujionyesha ni Serikali inayongoja kushika medani za utawala.
Lowassa amekuwa akisisitiza kuwa aina siasa zinazoendelea ndani ya chama hicho ikiwemo matukio ya baadhi ya Wabunge wake kutamka maneno makali, kuonyesha video zisizo na mashiko au kutaka kuzigeuza mahakama ni uwanja wa siasa haitawasaidia kufikia malengo yao.
Katika nasaha zake huku akiwaelekeza wenzake, Lowassa amesema bila chama hicho kupata msaada wa kuungwa mkono na vyombo vya nje na ndani vikiwemo vile vya ulinzi na usalama, kutakuwa na kazi ngumu ya kuungwa mkono hadi kukiangusha Chama Vha Mapinduzi.
Akizungumza na kutoonyesha kwake kufurahia matamshi ya Mwenyekiti Freeman Mbowe aliiyevishutumu hadharani vyombo vya ulinzi na usalama, akivinyooshea kidole cha tuhuma na shutuma ya kuhusika kupigwa risasi Mbunge Tundu Lissu, inaelezwa Lowassa hakupendezwa na madai hayo.
Aidha hata mkanda wa kuungaunga matukio yasiofiirika ulioonyeshwa na Mbunge Joshua Nassari ukidai kulikuwa na mazingira ya utoaji na upokeaji rushwa, amesema hauwezi kuwaaminisha Watanzania kama jambo hilo lina ukweli, uhalisia na si la kipropaganda zaidi.
Mbowe akionyesha ukomavu wa kisiasa wakati fulani amewahi kumkanya Nassari aliposimama kwenye jukwaa la mkutano wa kampeni huko Arumeru Mashariki, aliposema CCM haiungwi mkono kanda ya kaskazini hivyo ipo haja kwa Chadema kujitangazia himaya yao itakayotambuliwa kimataifa .
Mwenyekiti Mbowe aliwaambia Nassari kabla hujapanda jukwani aanza kutafakari, na ikibidi kuuliza mambo kuliko kuropoka na kusema mambo ya kitoto.
Baadhi ya wanasiasa wasomi na wenye uzoefu katika mambo ya utawala bado hawaridhishwi na siasa za wabunge Godbless Lema, Nassari, John Mnyika, John Heche , Halima Mdee, Joseph Mbilinyi na Ester Bulaya kutokana na kuonekana kujawa papara kuliko upangaji mikakati.
Hata hivyo maoni hayo ya Lowassa yamekuwa yakipingwa na PM Mstaafu Fredrick Sumaye ambaye amezusha mjadala ndani ya Chadema unaohoji kwanini Serikali ya Rais Dk Magufuli ishindwe kutaifisha mali na mashamba ya Lowassa na kuandamwa yeye peke yale huku akimtuhumu Lowassa kuwa na ukaribu na Dk Magufuli.
Maelezo na madai ya Sumaye anasema hana mali za kutisha wala mashamba aliyoyapata kwa njia za uporaji kuliko yale anayoyamiliki Lowassa ila ameshangazwa na uamuzi wa serikali kusakamwa yeye na mwenyekiti Mbowe huku Lowassa akiogopwa .
Pia Sumaye amesema wakati kukiwa na juhudi za kuvituhumu vyombo vya ulinzi na usalama katika tukio la kushambuliwa kwa risasi Tundu Lissu, ametaka ni heri Scotland Yard waitwe ili kufanya upelelezi ndani ya Chadema ikiwa Serikali haitaki.
Amesema haamini kwa asilimia nyingi iwapo hakuna njama hatari zilizopangwa ndani ya Chadema kwa upande mmoja , upande wa pili akitoa asilimia kidogo na kumtuhumu mtu mmoja aliyekataa kumtaja jina ndani ya Serikali na si kutovihusisha vyombo vyote vya ulinzi na usalama katika tukio hilo.
Mahali sakata hilo lilipofikia hivi sasa ndani ya Chadema kunafananishwa kama kuanza kwa ile vita au msokotano wa manahodha wanaopigania kushika SUKANI wakiwa katikati ya kina cha Bahari kabla ya kutia nanga kwa Jahazi lao kwenye ukingo wa bandari.
Hivi sasa hakuna tena siri ya kuficha jambo hilo au hitilafu zilizopo kutokana na viongozi wake muhimu kugawanyika hali iliyowasukuma hata Wanachama nao kila mmoja kuchagua na kufuata kundi au upande anaouona una manufaa kisiasa kwake .
Upo ushahidi wa moja kwa moja usemao Waziri Mkuu aliyejiuzulu kwa Kashfa ya Richmond Edward Lowassa, amerudia tena indhar yake akiwataka viongizi wenzake wa Chadema kujibadili toka kwenye kundi la uanaharakati ili kujigeuza na kuonekana ni kikosi adili cha Wanasiasa.
Kwa mara ya kwanza Lowassa alipotoa matamshi hayo alizusha tashwish na maneno mengi ndani ya Chadema huku baadhi ya viongozi hadi kufikia kumwambia yeye si mwalimu wa siasa wa kuifundisha Chadema na viongozi wake hivyo akubaliane na utamaduni wa Chama hicho au arudi CCM.
Lowassa akaonywa akitakiwa asijifanye Mwalimu Julius Nyerere ndani ya Chadema. Lowassa akubali na ashukuru kukaribishwa, kupewa nafasi ya kuwania urais mwaka 2015 ila akitakiwa awaachie chama chao kama alivyokikuta.
Madai ya Lowassa yanawataka wenzake wajitahidi kukiweka chama hicho katika mikono salama ya kuheshimika mbele ya Jumuiya za Kimataifa, Mashirika ya kidunia pia kiweze kuzivutia nchi wahisani, viongozi wa madhehebu za dini kwa kujionyesha ni Serikali inayongoja kushika medani za utawala.
Lowassa amekuwa akisisitiza kuwa aina siasa zinazoendelea ndani ya chama hicho ikiwemo matukio ya baadhi ya Wabunge wake kutamka maneno makali, kuonyesha video zisizo na mashiko au kutaka kuzigeuza mahakama ni uwanja wa siasa haitawasaidia kufikia malengo yao.
Katika nasaha zake huku akiwaelekeza wenzake, Lowassa amesema bila chama hicho kupata msaada wa kuungwa mkono na vyombo vya nje na ndani vikiwemo vile vya ulinzi na usalama, kutakuwa na kazi ngumu ya kuungwa mkono hadi kukiangusha Chama Vha Mapinduzi.
Akizungumza na kutoonyesha kwake kufurahia matamshi ya Mwenyekiti Freeman Mbowe aliiyevishutumu hadharani vyombo vya ulinzi na usalama, akivinyooshea kidole cha tuhuma na shutuma ya kuhusika kupigwa risasi Mbunge Tundu Lissu, inaelezwa Lowassa hakupendezwa na madai hayo.
Aidha hata mkanda wa kuungaunga matukio yasiofiirika ulioonyeshwa na Mbunge Joshua Nassari ukidai kulikuwa na mazingira ya utoaji na upokeaji rushwa, amesema hauwezi kuwaaminisha Watanzania kama jambo hilo lina ukweli, uhalisia na si la kipropaganda zaidi.
Mbowe akionyesha ukomavu wa kisiasa wakati fulani amewahi kumkanya Nassari aliposimama kwenye jukwaa la mkutano wa kampeni huko Arumeru Mashariki, aliposema CCM haiungwi mkono kanda ya kaskazini hivyo ipo haja kwa Chadema kujitangazia himaya yao itakayotambuliwa kimataifa .
Mwenyekiti Mbowe aliwaambia Nassari kabla hujapanda jukwani aanza kutafakari, na ikibidi kuuliza mambo kuliko kuropoka na kusema mambo ya kitoto.
Baadhi ya wanasiasa wasomi na wenye uzoefu katika mambo ya utawala bado hawaridhishwi na siasa za wabunge Godbless Lema, Nassari, John Mnyika, John Heche , Halima Mdee, Joseph Mbilinyi na Ester Bulaya kutokana na kuonekana kujawa papara kuliko upangaji mikakati.
Hata hivyo maoni hayo ya Lowassa yamekuwa yakipingwa na PM Mstaafu Fredrick Sumaye ambaye amezusha mjadala ndani ya Chadema unaohoji kwanini Serikali ya Rais Dk Magufuli ishindwe kutaifisha mali na mashamba ya Lowassa na kuandamwa yeye peke yale huku akimtuhumu Lowassa kuwa na ukaribu na Dk Magufuli.
Maelezo na madai ya Sumaye anasema hana mali za kutisha wala mashamba aliyoyapata kwa njia za uporaji kuliko yale anayoyamiliki Lowassa ila ameshangazwa na uamuzi wa serikali kusakamwa yeye na mwenyekiti Mbowe huku Lowassa akiogopwa .
Pia Sumaye amesema wakati kukiwa na juhudi za kuvituhumu vyombo vya ulinzi na usalama katika tukio la kushambuliwa kwa risasi Tundu Lissu, ametaka ni heri Scotland Yard waitwe ili kufanya upelelezi ndani ya Chadema ikiwa Serikali haitaki.
Amesema haamini kwa asilimia nyingi iwapo hakuna njama hatari zilizopangwa ndani ya Chadema kwa upande mmoja , upande wa pili akitoa asilimia kidogo na kumtuhumu mtu mmoja aliyekataa kumtaja jina ndani ya Serikali na si kutovihusisha vyombo vyote vya ulinzi na usalama katika tukio hilo.
Mahali sakata hilo lilipofikia hivi sasa ndani ya Chadema kunafananishwa kama kuanza kwa ile vita au msokotano wa manahodha wanaopigania kushika SUKANI wakiwa katikati ya kina cha Bahari kabla ya kutia nanga kwa Jahazi lao kwenye ukingo wa bandari.