Ujinga wa kitanzania kabisa!Mimi nafurahi kusikia na kuona yanayotukia.! Maana kipindi kile anaanza watu wakasema anawakomesha praise team ya Mwendazake, kwa hiyo wao wakajipa umuhimu kwa mtu asiewahusu. Wacha wanyooshwe, mpaka wajue nini wanasimamia.
Hii iwe work up call kwa upinzani na wapenda maendeleo na mabadiliko wasiojihusisha na CCM.
Yaani mtu from chama kile kile uongozi ule ule mlioulalamikia eti leo anakuwa mzuri kwa mambo machache alofanya tena within short term.
Bora hata ingekuwa kuna interval kidogo you can celebrate otherwise ilikuwa ni kujilisha upepo.
Nasema hivi wanyooshwe mpaka akili ziwakae sawa.
Nadhani hata huko Mwanza hakuna kitu wananchi watafanya maana hawajawahi kuwa na msimamo mmoja. Na leo inaenda kuwa siku ya mwisho kukutanika kisiasa.
Vinginevyo huenda Mbowe ni kada mtiifu wa CCM.
Eid Njema.