MIMI BABA YENU
JF-Expert Member
- Mar 1, 2019
- 319
- 755
Kumekuwa na UPOTOSHAJI mkubwa wa sakata la kuzuiwa kwa Makamu Mwenyekiti mpya wa Chadema John Heche Kufanya MKUTANO wa hadhara bila kufuata Utaratibu (kibali), Jimbo la Mbarali mkoani Mbeya tar 25/3/2025.
Ni kweli kabisa Jeshi la Polisi limemzuia Makamu Mwenyekiti bara Mhe. John Heche kuzungumza na wananchi wa jimbo la Mbarali. Mhe. Heche leo tarehe 25 Machi 2025 alikuwa amepanga Kufanya MKUTANO katika jimbo hilo kuendelea na Operesheni yao ya No Reforms No Election.
SHERIA NA TARATIBU ZA KUFUATWA ILI KUFANYA MIKUTANO.
Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977, kila Mtanzania anao uhuru wa kukutana kwa hiari na amani hivyo mikutano ya vyama vya siasa ni haki ya kikatiba kwa mujibu wa Ibara ya 20(1).
Lakini ili upata haki hii ya KIKATIBA ni lazima ufuata sheria zilizotungwa na Bunge ni pamoja na Sheria ya Vyama vya Siasa, Sura ya 258 (The Political Parties Act, Cap. 258) Kifungu cha 9(1)(c).
Chama cha siasa kitakuwa na haki ya kufanya mikutano ya hadhara kwa mujibu wa sheria zilizopo, Na Kifungu cha 11(1) na (3).
"Hakuna mtu yeyote atakayekizuia chama cha siasa kilichosajiliwa kuendesha shughuli zake kwa mujibu wa sheria hii."
Kwamba ili mikutano ya vyama vya siasa iweze kufanyika lazima ifuate Sheria na taratibu zilizowekwa.
Taratibu zinazotakiwa kufuatwa ni pamoja na Sheria ya Jeshi la Polisi kwa Huduma za Usalama, Sura ya 322 Kifungu cha 43
"Jeshi la Polisi lina wajibu wa kulinda mikutano ya hadhara baada ya kupokea TAARIFA YA KUSUDIO LA KUFANYIKA KWA MKUTANO KABLA YA MASAA 48"
CHADEMA wamepeleka TAARIFA ya kufanyika mkutano MASAA 12 kabla ya Mkutano kufanyika kinyume kabisa na Sheria ya Jeshi la Polisi.
Ni kweli kabisa Jeshi la Polisi limemzuia Makamu Mwenyekiti bara Mhe. John Heche kuzungumza na wananchi wa jimbo la Mbarali. Mhe. Heche leo tarehe 25 Machi 2025 alikuwa amepanga Kufanya MKUTANO katika jimbo hilo kuendelea na Operesheni yao ya No Reforms No Election.
SHERIA NA TARATIBU ZA KUFUATWA ILI KUFANYA MIKUTANO.
Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977, kila Mtanzania anao uhuru wa kukutana kwa hiari na amani hivyo mikutano ya vyama vya siasa ni haki ya kikatiba kwa mujibu wa Ibara ya 20(1).
Lakini ili upata haki hii ya KIKATIBA ni lazima ufuata sheria zilizotungwa na Bunge ni pamoja na Sheria ya Vyama vya Siasa, Sura ya 258 (The Political Parties Act, Cap. 258) Kifungu cha 9(1)(c).
Chama cha siasa kitakuwa na haki ya kufanya mikutano ya hadhara kwa mujibu wa sheria zilizopo, Na Kifungu cha 11(1) na (3).
"Hakuna mtu yeyote atakayekizuia chama cha siasa kilichosajiliwa kuendesha shughuli zake kwa mujibu wa sheria hii."
Kwamba ili mikutano ya vyama vya siasa iweze kufanyika lazima ifuate Sheria na taratibu zilizowekwa.
Taratibu zinazotakiwa kufuatwa ni pamoja na Sheria ya Jeshi la Polisi kwa Huduma za Usalama, Sura ya 322 Kifungu cha 43
"Jeshi la Polisi lina wajibu wa kulinda mikutano ya hadhara baada ya kupokea TAARIFA YA KUSUDIO LA KUFANYIKA KWA MKUTANO KABLA YA MASAA 48"
CHADEMA wamepeleka TAARIFA ya kufanyika mkutano MASAA 12 kabla ya Mkutano kufanyika kinyume kabisa na Sheria ya Jeshi la Polisi.