kitalembwa
JF-Expert Member
- Jul 12, 2014
- 6,171
- 15,862
Unakuta mtu mlisoma wote, pengine std. 7, form 4, au chuo, kitambo mlishapotezana, anaanza kukutafuta kwa kasi ya 5G, anataka mchango! Msg haziishi, mara kupigiwa simu!
Unajikuta ghafla new WhatsApp group heading "mchango wa... ." Mimi nikiona hivyo huwa naleft haraka sana, mtu anakamomaa kukucheki manually, namjibu simpo tu sina pesa kwa sasa! Sitoi ahadi maana itakuwa usumbufu usiokoma!
Harusi michango, send-off michango, kitchen party michango, kipaimara michango, komunio michango, jubilei michango, engagement michango!
Sikatai kuwa dhana ya kufanya sherehe/shughuli ama tafrija ni kuweka umoja hususani ndugu, marafiki n.k Lakini mwenye sherehe akijiona hana uwezo wa kukidhi hayo kwa nini asumbue watu wamchangie? Nimeshuhudia watu kadhaa wanafilisika ama kuingia katika madeni kwa sababu tu ya kufanya sherehe ili afurahishe watu!
Binafsi hizi habari za michango sina habari nazo kabisa, huwa natoa jibu la moja kwa moja, sina pesa! Huwa nachangia misiba tu, tena huwa naangalia, sio misiba yote nachanga. Unakuta mtu ni jirani yako, amefiwa na ndugu wa mke wake, anaenda kijijini kuzika, nakupaje mchango?
Unajikuta ghafla new WhatsApp group heading "mchango wa... ." Mimi nikiona hivyo huwa naleft haraka sana, mtu anakamomaa kukucheki manually, namjibu simpo tu sina pesa kwa sasa! Sitoi ahadi maana itakuwa usumbufu usiokoma!
Harusi michango, send-off michango, kitchen party michango, kipaimara michango, komunio michango, jubilei michango, engagement michango!
Sikatai kuwa dhana ya kufanya sherehe/shughuli ama tafrija ni kuweka umoja hususani ndugu, marafiki n.k Lakini mwenye sherehe akijiona hana uwezo wa kukidhi hayo kwa nini asumbue watu wamchangie? Nimeshuhudia watu kadhaa wanafilisika ama kuingia katika madeni kwa sababu tu ya kufanya sherehe ili afurahishe watu!
Binafsi hizi habari za michango sina habari nazo kabisa, huwa natoa jibu la moja kwa moja, sina pesa! Huwa nachangia misiba tu, tena huwa naangalia, sio misiba yote nachanga. Unakuta mtu ni jirani yako, amefiwa na ndugu wa mke wake, anaenda kijijini kuzika, nakupaje mchango?