Mheshimiwa Kikwete, omba radhi watanzania

mcfm40

JF-Expert Member
Nov 2, 2010
4,452
3,150
Ni uungwana tu kama mheshimiwa Kikwete utaomba radhi kwa watanzania hapo kesho kwani ndio muda muafaka na nafasi pekee ya kufanya hivyo.

Omba radhi watanzania kwa kuifanya hii nchi kukosa mwelekeo na kuwa shamba la bibi. Mara nyingi tumemsikia rais Magufuli akilalamika kwamba hii nchi ililiwa sana, huko serikalini mambo yaliyokuwa yanafanyika yalikuwa ya hovyo, na akasema anaposema ya hovyo ni ya hovyo kwelikweli, kwamba hii nchi ilikuwa shamba la bibi.

Haya maneno ameyasema kwa kuyarudiarudia huyu unayemkabidhi madaraka ya chama leo.

Ili kuonesha basi unamuunga mkono mh rais na mwenyekiti mpya, na kwamba anayoyaongea ni kweli na si porojo za kisiasa, omba radhi. Usipofanya hivyo wenye akili zetu tutajiuliza mengi sana. Na tutaamini kwamba hizi ni mbinu za chama chenu kuwarubuni wstanzania.

Ama ukubaliane na Magufuli kwa kutuomba radhi watanzania au ukanushe kwamba hukufanya hii nchi shamba la bibi na tumbuatumbua inayoendelea ni utaratibu wa kawaida wa uongozi mpya kujipangia safu yao na si kweli kwamba ni wabadhirifu kama wanavyosemwa na mh rais!

Usipofanya hivyo basi wewe na chama chako mtakuwa mmewadharau sana watanzania na haya mnayofanya sasa yatakuwa ni maigizo tu!
 
Kesho mie najua atakuwa anacheka tu au kutoa tabasamu lake kwa sanaaaaaa. Hiyo ni moja ya kumbukumbu kubwa juu yake, na pia namisi kusoma habari za leo raisi wa nchi yangu hii kasafiri yupo nchi gani. Pia kuangalia picha za Issa Michuzi akirusha huku wa ikulu akiwa analipwa tu mshahara, na kupiga holidays za nguvu bila kazi kubwa ya kufanya.
 
Tulichemka wenyewe tu Leo kila mtu anasema JPM atalekebisha mapungufu maana wanakilli udhaifu wa jamaa
 
Ni uungwana tu kama mheshimiwa Kikwete utaomba radhi kwa watanzania hapo kesho kwani ndio muda muafaka na nafasi pekee ya kufanya hivyo.

Omba radhi watanzania kwa kuifanya hii nchi kukosa mwelekeo na kuwa shamba la bibi. Mara nyingi tumemsikia rais Magufuli akilalamika kwamba hii nchi ililiwa sana, huko serikalini mambo yaliyokuwa yanafanyika yalikuwa ya hovyo, na akasema anaposema ya hovyo ni ya hovyo kwelikweli, kwamba hii nchi ilikuwa shamba la bibi.

Haya maneno ameyasema kwa kuyarudiarudia huyu unayemkabidhi madaraka ya chama kesho/leo.

Ili kuonesha basi unamuunga mkono mh rais na mwenyekiti mpya, na kwamba anayoyaongea ni kweli na si porojo za kisiasa, omba radhi. Usipofanya hivyo wenye akili zetu tutajiuliza mengi sana. Na tutaamini kwamba hizi ni mbinu za chama chenu kuwarubuni wstanzania.

Ama ukubaliane na Magufuli kwa kutuomba radhi watanzania au ukanushe kwamba hukufanya hii nchi shamba la bibi na tumbuatumbua inayoendelea ni utaratibu wa kawaida wa uongozi mpya kujipangia safu yao na si kweli kwamba ni wabadhirifu kama wanavyosemwa na mh rais!

Usipofanya hivyo basi wewe na chama chako mtakuwa mmewadharau sana watanzania na haya mnayofanya sasa yatakuwa ni maigizo tu!
We umefanya ya hovyo mangapi na umemuomba radhi nani?.
 
Nakumbuka aliwahi kujigamba kwamba anataka akiondoka madarakani akumbukwe kwa jina la bwana maendeleo! Leo Magufuli amembatiza Bwana Failure!
 
We umefanya ya hovyo mangapi na umemuomba radhi nani?.
Naam mimi kila nikifanya la hovyo naomba radhi! Bahati mbaya mimi sio public figure hivyo ya hovyo yangu hayaiumizi public na wewe pia huwezi kujua km nimeomba radhi!
 
Tatizo wengi wenu kipindi cha mkapa mlikuwa hamjui chochochote
Ebo, si mimi niliyesema hayo. Nimemquote tu Magu. Unamaanisha Magu anapolaumu uongozi wa Kikwete kwa kuifanya nchi shamba la bibi hajui kitu?
 
Umeongea pumba tupu vitu vyote unavyo viona now ameleta jk... hakuna rais aliethubutu na kufanya kama kikwete..
Sasa kwa nini Magu anadai eti uongozi wake uliifanya nchi km shamba la bibi? Ndio nasema Kikwete asimame aseme wazi kwamba anaonewa!
 
Itasaidia nini..!? haliyakuwa hakiwezi kurudi chochote kilicholiwa.
 
Back
Top Bottom