Pamoja na UKAWA kuwa ni wa vyama vya upinzani, lakini katika hili wameonyesha kidogo uzalendo wa kupigania maoini ya wananchi.
Ni kawaida ya ccm kutengeneza tatizo halafu wakijidai kulimaliza sisi wananchi tunawapigia makofi - eti serikali sikivu!!!!Ni kweli Sita aliingizwa mkenge,mkuu wa kaya ndiye chanzo cha sakata lote hili,na sasa watu wanampongeza kwa kitu ambacho alijua mwisho wa siku kitakwama na yeye ndiye mkwamuaji,watanzania fungueni macho
Imekuaje leo mwanaCCM unakubaliana na UKAWA au hii sredi kuna mtu ameandika kwa niaba yako?
Umepewa nafasi ya kufanya uchaguzi na kupata wajumbe wapya kwa bmk lijalo. Ni juu yako kuwaondoa hao waliopindisha mawazo ya wananchi na kuweka ya kwao. Hii ni fursa nzuri - tuitumie.
Usisahau pia kuwa tutakuwa na rais mwingine ambaye si lazima aje na mawazo kama ya JK. Kumbuka mbunge mmoja aliwahi kusema " anayeshikila nguvu za dola (instruments of power) ndiye mwenye uwezo wa kusema katiba mpya iwepo na ikawa au sitaki katiba mpya na ikawa. Alitoa mfano wa Afrika ya kusini
Pigo siyo kwa Sitta maana yeye alipewa maelekezo kasimamie moja, mbili, tatu.........hicho kikundi kilichotoa maelekezo ya mpaka Raisi afungue Bunge baada ya Rasimu kuwasilishwa na kufutilia mbali tovuti ya Tume ingefaa hiyo majina yao yawekwe wazi ili Watanzania wawafahamu.
Mimi wa kwanza ni Waziri wa Katiba na Sheria - Asha Rose Migire, Tovuti iko wizarani kwake
Sita kama mwanasesere tu!
Masikini Mzee Sitta......Kajiabisha mpaka namuonea huruma..