Jana (08/05/2012) katika taarifa ya habari ya saa mbili usiku kupitia ITV, mtangazaji Renatus Mubabuzi aliripoti juu ya kuharibika kwa mkokoteni uliokuwa unatumiwa na wananchi wa Kiromba/Nanyamba, Wilaya na Jimbo la Mtwara Vijijini kwa ajili ya kuwabebea wagonjwa na kuwapeleka katika vituo vikubwa vya afya.
Mganga Mfawidhi wa Zahanati hiyo aliiomba serikali iwasaidie gari la kubebea wagonjwa, lakini hata Pikipiki ingewafaa tu.Habari zilipasha kuwa mkokoteni ule ulioharibika, ulikuwa unategemewa na vijiji vipatavyo vinane.
Mh. Hawa Ghasia, tunakuomba utekeleze ahadi zako na pia ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 ( 66(j))
Mganga Mfawidhi wa Zahanati hiyo aliiomba serikali iwasaidie gari la kubebea wagonjwa, lakini hata Pikipiki ingewafaa tu.Habari zilipasha kuwa mkokoteni ule ulioharibika, ulikuwa unategemewa na vijiji vipatavyo vinane.
Mh. Hawa Ghasia, tunakuomba utekeleze ahadi zako na pia ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 ( 66(j))