Hivi ni visa vya mbaazi.
Ni vizuri huyo waziri akajaribu kupanua wigo wa ubongo wake. Asidhani kwamba kwa kuwa ccm imewekeza katika ujinga basi watanzania wataendelea kuwa majuha wasijitambue siku zote.
Madreva wametoa malalamiko yao, serikali imeyasikiliza na hatimaye mara mbili kutamka kwamba ni madai halali na serikali imeona kuna hoja za kushughulikia. Huo uchochezi leo umetoka wapi?
Kwamba wamechochewa kujua haki zao au wamechochewa kutambua kwamba maisha yao yanashida na wanazidi kuumizwa?
Hainiingii akilini kwamb atuna mawaziri wa kiwango kile.
Mtu akiwa anaumwa kichwa, maumivu makali hadi anatoa machozi, kuna hitaji mtu wa kumchochea ili ajue kichwa chake kinamuuma? Machozi yanapomtoka kwa maumivu, utakuwa na akili timamu ukiacha kumtafutia tiba kama unamjali, au kuanza kutafuta nani kamwambia atoe machozi? Kwamba kulia machozi ya maumivu hadi kuwepo mchochezi?
Huu sasa ni zaidi ya wendawazimu!.
Madreva, waoneni hao mawaziri wa ccm walivyo na nia ovu, ufahamu mdogo huku wamejaa hila. Juzi walisema kinafiki kwamba shida zenu ni za kweli. Leo wamekaa kimya hawataki kutafuta suluhu, wanatafuta nani aliyewaambia mseme mnaumia!. Ni dharau iliyoje? Kwa mtaji huo, ni dhahiri Chama Cha Mapinduzi, kimewafanya Watanzania matutuso wasiojitambua hata wangeumizwaje, wabaki wakicheka cheka na kupiga makofi ya ahsante. Na kwamba hawatakiwi kujitambua na kujitambua ama kueleza maumivu ni sawa na msukule kaasi kambi, anatafutwa aliyemzindua!.
KUNA SABABU GANI JAMANI YA KUENDELEA KUONGELEA SERIKALI YA CCM? WATANZANIA AMKENI. CCM INATAKIWA IONDOLEWE OCTOBER, VINGINEVYO MTAKUWA MISUKULE ISYOTAKIWA KUTUMIA AKILI NINYI NA WATOTO WENU WOTE!.
Waziri amaeudhi.