JT2014
JF-Expert Member
- Jan 18, 2014
- 1,863
- 1,374
Wana janvi naamini nyote mu-wazima.
Naomba tujadili au naomba kujua kwa anayefahamu anifafanulie
dhana kamili ya mwenge ambao hupewa heshima kubwa hapa nchini
na kutumia fedha nyingi katika mbio zake huku madarasa ya wanafunzi
hayana madawati na vitu muhimu mashuleni.
Ukiangalia mabango yote yanayomnadi mgombea huyo
utaona katika herufi ya kwanza ya jina la mgombea yaani M imebeba alama ya mwenge,
Na ni kila bango na kipeperushi,swali langu ni nini uhusiano wa chama hiki
au nchi hii na mwenge? Je mwenge ni alama ya kisiasa au alama ya kiimani?
Tumekuwa tukiaminishwa kwamba nchi hii haina dini,
na kweli jambo hili linasifika kututengenezea amani ya nchi
ila najiuliza je mwenge ni nini? maana hakuna sababu ya kisayansi
inayothibitisha uwepo wa faida za Mwenge.Zamani Tuliambiwa unaleta matumaini N.k
Mambo hayo hayana uthibitisho kisayansi bali kiimani,je imani hiyo ni ya dini gani
maana serikali haina dini ila watu wake wana dini.
Kama mwenge hauna uthibitisho wa kisayansi kuleta matumaini
bali imani,na imani hii si ya dini yoyote bali ni imani ya asili
je dini ya serikali au ni imani ya asili? Na kama jibu ni ndiyo
tunaweza kupinga vitendo vinavyoambatana na imani za asli ambazo
tunaziita za kishirikina?
Binafsi siungi mkono matumizi ya mwenge
ambao hatuelewi unatumia imani gani?
La kushangaza ni nembo muhimu kwenye
mabango ya mgombea wa chama tajwa hapo juu
Karibuni nyote mnieleweshe.
Naomba tujadili au naomba kujua kwa anayefahamu anifafanulie
dhana kamili ya mwenge ambao hupewa heshima kubwa hapa nchini
na kutumia fedha nyingi katika mbio zake huku madarasa ya wanafunzi
hayana madawati na vitu muhimu mashuleni.
Ukiangalia mabango yote yanayomnadi mgombea huyo
utaona katika herufi ya kwanza ya jina la mgombea yaani M imebeba alama ya mwenge,
Na ni kila bango na kipeperushi,swali langu ni nini uhusiano wa chama hiki
au nchi hii na mwenge? Je mwenge ni alama ya kisiasa au alama ya kiimani?
Tumekuwa tukiaminishwa kwamba nchi hii haina dini,
na kweli jambo hili linasifika kututengenezea amani ya nchi
ila najiuliza je mwenge ni nini? maana hakuna sababu ya kisayansi
inayothibitisha uwepo wa faida za Mwenge.Zamani Tuliambiwa unaleta matumaini N.k
Mambo hayo hayana uthibitisho kisayansi bali kiimani,je imani hiyo ni ya dini gani
maana serikali haina dini ila watu wake wana dini.
Kama mwenge hauna uthibitisho wa kisayansi kuleta matumaini
bali imani,na imani hii si ya dini yoyote bali ni imani ya asili
je dini ya serikali au ni imani ya asili? Na kama jibu ni ndiyo
tunaweza kupinga vitendo vinavyoambatana na imani za asli ambazo
tunaziita za kishirikina?
Binafsi siungi mkono matumizi ya mwenge
ambao hatuelewi unatumia imani gani?
La kushangaza ni nembo muhimu kwenye
mabango ya mgombea wa chama tajwa hapo juu
Karibuni nyote mnieleweshe.