Mgombea Urais wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Salum Mwalimu na mgombea mwenza wake, Devotha Minja, wakiongoza kazi ya kuandikisha wadhamini wao leo mkoani Lindi.
Mgombea huyo wa CHAUMMA ameanza leo ziara katika mikoa mbalimbali ya kuomba udhamini wa kupeperusha bendera katika nafasi hiyo ya Urais kwenye uchaguzi mkuu mwaka huu.