issenye
JF-Expert Member
- Feb 2, 2011
- 3,795
- 5,255
Mgombea Ubunge wa jimbo la Siha kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Godwin Mollel amefarijika kuona bendera ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwenye mkutano wake wa Makiwalu wakati akifanya kampeni za kugombea Ubunge wa jimbo.
"Niwaambie makamanda bado nina wapenda na kuwaheshimu ndiyo maana nimefarijika kuona bendera hizi mbili (CHADEMA) na (CCM) zipo hapa lakini mmeniwekea kwa namna nzuri kwamba mmeiweka ile juu na mmeonyesha dalili kwamba tutaishusha hii ya chini tuendelee kujenga Siha, mimi leo ni limao nimekuja kuondoa kichefu chefu cha maendeleo na watu wapate maendeleo" alisema Mollel Mbali na hilo Dkt. Mollel amedai kuwa anakumbuka mchango wa makanda hao ambao waliweza kusimama na yeye na kulinda kura mpaka siku alipotangazwa kuwa Mbunge wa jimbo la Siha kupitia CHADEMA.
Chanzo: IPP Media
"Niwaambie makamanda bado nina wapenda na kuwaheshimu ndiyo maana nimefarijika kuona bendera hizi mbili (CHADEMA) na (CCM) zipo hapa lakini mmeniwekea kwa namna nzuri kwamba mmeiweka ile juu na mmeonyesha dalili kwamba tutaishusha hii ya chini tuendelee kujenga Siha, mimi leo ni limao nimekuja kuondoa kichefu chefu cha maendeleo na watu wapate maendeleo" alisema Mollel Mbali na hilo Dkt. Mollel amedai kuwa anakumbuka mchango wa makanda hao ambao waliweza kusimama na yeye na kulinda kura mpaka siku alipotangazwa kuwa Mbunge wa jimbo la Siha kupitia CHADEMA.
Chanzo: IPP Media