mwankuga
JF-Expert Member
- Aug 30, 2010
- 334
- 120
Kwa zaidi ya miezi minne, nchi iko kwenye mgawo mkubwa wa umeme.Tanesco wamekuwa wakijitokeza kutoa taarifa (japo kwa kusuasua), kueleza sababu ya mgawo huo, na mikakati ya kukabiliana na suala hilo.
Mara ya kwanza tuliambiwa, mgawo wa umeme ungepungua au kuisha baada ya kukamilisha kuunganisha umeme wa gesi kwenye gridi ya Taifa.Hali ya umeme ingeimarika wiki ya pili ya mwezi Agosti.
Badala yake, hali imekuwa mbaya zaidi kuliko awali, na sababu ni tofauti na za awali.Sasa hivi tunazungumzia ukame.Mabwawa ya kuzalisha umeme, yamepunguza uwezo wa kuzalisha umeme.
Bila shaka hali ni mbaya.Wagombea wa urais (Lowassa na Magufuli), kwa kiasi wanaishutumu TANESCO.Lakini najiuliza hivi Tanesco wanapenda kuwepo na mgawo wa umeme?Bila shaka hawapendi, lakini hali halisi inawalazimu kufanya hivyo.Sasa nani alaumiwe kwa hili tatizo?Kwa bahati mbaya Tanesco (wafanyakazi), wanayo mengi ya kusema, lakini hawana jukwaa la kusemea.
Wanasiasa ndio waliotufikisha hapa tulipo.Ndio wameifanya Tanesco kushindwa kufanya kazi yake kwa ufanisi,kwa kuingia mikataba ya hovyo kabisa,kuwahi kusainiwa duniani.
Wakati tunasubiria Oktoba 25, ni muhimu mpiga kura kutafakari haya.Waliosababisha hali hii hawapaswi kupewa nafasi tena.Piga kura ya Mabadiliko.