Mganga wa kienyeji anahitajika

ZamdaIssa

JF-Expert Member
Nov 10, 2015
879
1,456
Wadau sallam kwenu wote!!kwanza sinahaja ya kuja na ID fake!!naandika na hii hii ya miaka yote,atakaenichukulia tofauti atajua mwenyewe sijali wala nini!!

Jamani tunamgonjwa kwetu,tumeuguza tumemaliza mahospital makubwa hapa bongo ugonjwa hauonekani!!ana miezi 6 sasa amelala tu kitandani munamnyanyua!!tumemaliza vipimo,CT Scan,MRI na takataka zote za Figo,Ini,visukari na pressure hakuna walichopata!!
.
Dar tumeimaliza,Arusha tumemaliza,Moshi KMC nayo tumemaliza hatujaambulia kitu

Wengi wanadai ndugu yetu karogwa!!mimi mswahili naamini katika holo kwakua hata katika dini uchawi upo!!Tumesoma visomo weee labda atapata nafuu ila hamna yupo vilevile!!
.
Sasa jamani kwa anaejua mganga nguli wa kienyeji anielekeze jamani,iwe Tanga iwe sumbawanga iwe popote pale!!sina jinsi yamenifika shingoni!!
.
NB:wajuaji wa maombi siwataki tushamaliza makanisa,nataka waganga wa jadi,potelea mbali nikiibiwa ila mi nachotaka ni msaada!!hakuna sehemu mungu amesema tusitumie mizizi kujitibu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom