Meya awakalia kooni madiwani CHADEMA

Meya awakalia kooni madiwani CHADEMA

Rapkatuni

Member
Joined
Sep 27, 2011
Posts
29
Reaction score
5
Meya wa Manispaa ya Ilemela mkoani Mkoani Mwanza Henry Matata amesema kuwa uamuzi wa kuwafukuza madiwani watatu wa CHADEMA katika manipaa hiyo, upo pale pale.

Madiwani hao wamekumbwa na sokomoko hilo, kutokana na kushindwa kuhudhuria vikao vitatu mfululizo bila idhini ya mwenyekiti ambaye ni meya.

Akizungumza na MTANZANIA kwa njia ya simu akiwa mjini Dodoma, Matata alisema uamuzi wa kuwafukuza upo pale pale na kwamba hakuna mamlaka nyingine inayoweza kutengua.

Meya huyo alisema kuwa kinachosubiriwa kwa sasa ni kutangazwa kwa tarehe ya kufanyika uchaguzi mdogo katika kata tatu ambazo madiwani wake walifukuzwa kwa mujibu wa sheria.

Meya huyo ambae alifukuzwa CHADEMA kisha kufungua kesi mahakamani kupinga uamuzi wa Kamati Kuu (CC) alisema yeye hababaishwi na maneno.
 
Sema Mamluki Matata utaeleweka , Matata hajawahi kuwa Meya na hakuna siku atakuja kuwa meya ! hata yeye analifahamu hilo , anabebwa na Magamba kwa sababu ambazo hata wewe unazifahamu.
 
Fukuza...Ukifanyika uchaguzi CHADEMA watashinda tena tu, Nani atakula hasara hapo?
 
ni bora chadema ianze maandalizi ya uchaguzi kuliko kulumbana majukwaani
 
Meya wa Manispaa ya Ilemela mkoani Mkoani Mwanza Henry Matata amesema kuwa uamuzi wa kuwafukuza madiwani watatu wa CHADEMA katika manipaa hiyo, upo pale pale.

Madiwani hao wamekumbwa na sokomoko hilo, kutokana na kushindwa kuhudhuria vikao vitatu mfululizo bila idhini ya mwenyekiti ambaye ni meya.


Akizungumza na MTANZANIA kwa njia ya simu akiwa mjini Dodoma, Matata alisema uamuzi wa kuwafukuza upo pale pale na kwamba hakuna mamlaka nyingine inayoweza kutengua.

Meya huyo alisema kuwa kinachosubiriwa kwa sasa ni kutangazwa kwa tarehe ya kufanyika uchaguzi mdogo katika kata tatu ambazo madiwani wake walifukuzwa kwa mujibu wa sheria.

Meya huyo ambae alifukuzwa CHADEMA kisha kufungua kesi mahakamani kupinga uamuzi wa Kamati Kuu (CC) alisema yeye hababaishwi na maneno.



Hahahaha anadaiwa na chama m29 asipolipa magereza inamhusu awaulize madiwani waliofukuzwa arusha
 
Hili lina sura ya kisheria..,litaenda kisheria na kutolewa maamuzi on the basis of prevailing laws. Kama wapo wanaofikiri kuwa kelele za kisiasa zinabadili maamuzi ama zina nafasi katika vyombo vya dola na mamlaka za kufanya maamuzi watasubiri sana.
 
...hivi kesi ya hili "jidubwasha" matata imefikia wapi?...
 
  • Thanks
Reactions: ESI
Chadema wamemshindwa matata, hilo litawagharimu sana chadema!!
sema CCM waliompigia chapuo na kupindisha sheria walidhani wamepata kumbe wamepatikana , wamesimamisha maendeleo ya Ilemela bila sababu za msingi uongozi wa dotcom, wako radhi wananchi waumie ili wawafrustrate chadema matokeo yake MACCM mwanza wanaipata total public rejection
 
Hili lina sura ya kisheria..,litaenda kisheria na kutolewa maamuzi on the basis of prevailing laws. Kama wapo wanaofikiri kuwa kelele za kisiasa zinabadili maamuzi ama zina nafasi katika vyombo vya dola na mamlaka za kufanya maamuzi watasubiri sana.

Kama yeye alivyobaki kuwa na Diwani na Meya wakati alifukuzwa chama....ndivyo na hao madiwani watakavyorudi katika nafasi zao bila kufanyika uchaguzi mwingine....sheria ile ile iliyomuweka hapo...the same will stand for those councillors!
 
Back
Top Bottom