Nimesikia mahubiri ya Mchungaji Kimario akiwashangaa wazee wanaoshauri vijana wajiajiri.
Anasema wao wako serikalini miaka zaidi ya 30 hawajajiajiri wanawezaje kuwaambia vijana wanaotoka vyuo vikuu wajiajiri!
Binafsi ni mhanga wa ajira na nilishinikizwa sana na wazazi nitafute kazi ijapo nilipenda kufanya biashara sana.Bahati mbaya mama yangu hakunipa baraka zake katika biashara ndipo nikajitosa kwenye ajira na hadi leo nimekuwa mtumwa wa ajira.
Mimi namuunga mkono mchungaji huyo lakini naomba yeye awe wa kwanza kuacha kazi hiyo ya kulipwa ili vijana wafanye kazi. Anaweza kujiajiri kwa kuhubiri kama Mwalimu Mwakasege.
Ukitaka kufundisha somo ueleweke fundisha kwa mfano, vinginevyo tutamuona mtu anayetaka tu umaarufu rahisi kwa vijana wasiojielewa. Maana ni serikali gani inaweza kuajiri watu wote?
Anasema wao wako serikalini miaka zaidi ya 30 hawajajiajiri wanawezaje kuwaambia vijana wanaotoka vyuo vikuu wajiajiri!
Binafsi ni mhanga wa ajira na nilishinikizwa sana na wazazi nitafute kazi ijapo nilipenda kufanya biashara sana.Bahati mbaya mama yangu hakunipa baraka zake katika biashara ndipo nikajitosa kwenye ajira na hadi leo nimekuwa mtumwa wa ajira.
Mimi namuunga mkono mchungaji huyo lakini naomba yeye awe wa kwanza kuacha kazi hiyo ya kulipwa ili vijana wafanye kazi. Anaweza kujiajiri kwa kuhubiri kama Mwalimu Mwakasege.
Ukitaka kufundisha somo ueleweke fundisha kwa mfano, vinginevyo tutamuona mtu anayetaka tu umaarufu rahisi kwa vijana wasiojielewa. Maana ni serikali gani inaweza kuajiri watu wote?