ubongokid
JF-Expert Member
- Apr 30, 2017
- 2,265
- 4,453
Kwa huzuni naandika,Moyoni nahuzunika
Nikweli limenitokea,majuto ni mjukuu
Natamni rudi nyuma,Historia badilisha
Mchepuko niachie,Familia niijenge
Najua nilikosea,huba yako kuionja
Utamu nilinogewa,nikasahau wajibu
Penzi limetamalika,sasa nimekuwa Zoba
Mchepuko niachie,Familia niijenge
Kipato changu kidogo,kukutunza sitoweza
Majukumu yamebana.nahisi kutokwa roho
Natamani kula vyote,mfuko hauruhusu
Mchepuko niachilie,Familia niijenge
Kiuno chako cha nyigu,Na sura yako ya yai,
Ngozi yako yateleza,manukato yalewesha
Mavazi yako murua,si mtumba si spesho
Mchepuko niachilie,Familia niijenge
Maliwato mejaliwa,mbinukowo mwanana
Nikiushusha mkono,watulia palepale
Kiunocho ni chembamba,Namba nane yajichora
Mchepuko niachilie,familia niijenge
Kunako sitakwasita,bidiiyo naiona
Unanitoa utamu,kwa kweli unajituma
Mahabayo ni adimu,hakika umehitimu
mchepuko niachilie,familia niijenge
mdekewo wa pekee,walia kila sauti,
mara 'bebi' mar hani, yaani unanidatisha
Kama mahaba maradhi,basi mimi mahututi
mchepuko niachilie.familia niijenge
Mkasa umenikumba,kwa sasa ni njia panda
Mchepuko unang'ang'ana,wataka daima dumu
Mwenzenu nataka toka,nirudi kwa mke wangu
mchepuko niachie,familia niijenge
Makosa nilishakosa,Utamu nshaonjeshwa
Mitara sitoiweza,mmoja ananitosha
Kuchepuka si ujanja,Ila kwa sasa najuta
Mchepuko niachie,familia niijenge
Malenga nawauliza,nifanye nini mwenzeni
Mchepuko umegoma,wataka daima dumu
Nataka nihame mji kukimbia mchepuko
mchepuko nichilie,familia niijenge
Tamati nimefikia,mkasa bado kuisha,
bado nipo majangani,hali yangu napambana
Natamani jua suluhu,ya hili langu janga
Mchepuko niachie,familia niijenge
PBK
Nikweli limenitokea,majuto ni mjukuu
Natamni rudi nyuma,Historia badilisha
Mchepuko niachie,Familia niijenge
Najua nilikosea,huba yako kuionja
Utamu nilinogewa,nikasahau wajibu
Penzi limetamalika,sasa nimekuwa Zoba
Mchepuko niachie,Familia niijenge
Kipato changu kidogo,kukutunza sitoweza
Majukumu yamebana.nahisi kutokwa roho
Natamani kula vyote,mfuko hauruhusu
Mchepuko niachilie,Familia niijenge
Kiuno chako cha nyigu,Na sura yako ya yai,
Ngozi yako yateleza,manukato yalewesha
Mavazi yako murua,si mtumba si spesho
Mchepuko niachilie,Familia niijenge
Maliwato mejaliwa,mbinukowo mwanana
Nikiushusha mkono,watulia palepale
Kiunocho ni chembamba,Namba nane yajichora
Mchepuko niachilie,familia niijenge
Kunako sitakwasita,bidiiyo naiona
Unanitoa utamu,kwa kweli unajituma
Mahabayo ni adimu,hakika umehitimu
mchepuko niachilie,familia niijenge
mdekewo wa pekee,walia kila sauti,
mara 'bebi' mar hani, yaani unanidatisha
Kama mahaba maradhi,basi mimi mahututi
mchepuko niachilie.familia niijenge
Mkasa umenikumba,kwa sasa ni njia panda
Mchepuko unang'ang'ana,wataka daima dumu
Mwenzenu nataka toka,nirudi kwa mke wangu
mchepuko niachie,familia niijenge
Makosa nilishakosa,Utamu nshaonjeshwa
Mitara sitoiweza,mmoja ananitosha
Kuchepuka si ujanja,Ila kwa sasa najuta
Mchepuko niachie,familia niijenge
Malenga nawauliza,nifanye nini mwenzeni
Mchepuko umegoma,wataka daima dumu
Nataka nihame mji kukimbia mchepuko
mchepuko nichilie,familia niijenge
Tamati nimefikia,mkasa bado kuisha,
bado nipo majangani,hali yangu napambana
Natamani jua suluhu,ya hili langu janga
Mchepuko niachie,familia niijenge
PBK