Brigedia Chan-ocha
JF-Expert Member
- Mar 7, 2014
- 1,353
- 2,849
Hii imetokea Mwanza wiki iliyopita, kuna rafiki yangu tunaishi pamoja kama majirani, yaani nyumba yake na yangu zipo karibu sana. Nyumba aliyopanga ina wapangaji 5, sasa ni muda kidogo alianza kuwa na mahusiano na mke wa mpangaji mwenzake.
Sasa wiki iliyopita, mume wake majira ya saa 12 jioni alienda kuhani msiba mtaa wa pili, sasa rafiki yangu huyu na mke wa mpangaji mwenziye wakakubaliana kuwa waende bafuni, yaani mwanamke ajifanye kama anaenda kuoga alafu mwanaume ataenda aingie bafuni ili wafanye yao.
Sasa mwanamke akaingia bafuni then mwanaume akafuatia, ile wanaendelea kupeana mambo yao humo bafuni, mumewe akafika kutoka msibani na akawa anaeelekea uani kujisaidia, bafuni kuna dirisha, mchepuko ukawahi kumuona mume kwa haraka akamwambia mke wa mshikaji kuwa "mumeo anakuja" ile mke kumuona mumewe anakuja, haraka haraka ukafungua mlango wa bafuni ule mchepuko ukatoka haraka sana na kutumbukia kwenye mtaro wa maji machafu ukajibanza pembeni ya bafu, mlango wa bafuni ulisikika ukijigonga kwa sauti, mume alipofika uani akamuuliza mkewe kuwa "mbona unaoga muda mrefu"? mkewe akamjibu "ndo nimeingia bafuni sa hivi" (kwa sauti ya kutetemeka)
Baada ya kujisaidia mumewe alimulika-mulika huku na kule kwa tochi yake aliyokuwa nayo baadae akarudi ndani, huyu mshikaji anasema amekoma kabisa kumla mke wa jirani yake maana ilikuwa ni chupu chupu akamatwe na alipata michubuko wakati wa vurumai lile.
My take: Mke wa mtu ni hatari, kila mtu atafute wa kwake, sasa hivi vijana wengi hawaoi, wanavizia wake za wenzao tu.
Sasa wiki iliyopita, mume wake majira ya saa 12 jioni alienda kuhani msiba mtaa wa pili, sasa rafiki yangu huyu na mke wa mpangaji mwenziye wakakubaliana kuwa waende bafuni, yaani mwanamke ajifanye kama anaenda kuoga alafu mwanaume ataenda aingie bafuni ili wafanye yao.
Sasa mwanamke akaingia bafuni then mwanaume akafuatia, ile wanaendelea kupeana mambo yao humo bafuni, mumewe akafika kutoka msibani na akawa anaeelekea uani kujisaidia, bafuni kuna dirisha, mchepuko ukawahi kumuona mume kwa haraka akamwambia mke wa mshikaji kuwa "mumeo anakuja" ile mke kumuona mumewe anakuja, haraka haraka ukafungua mlango wa bafuni ule mchepuko ukatoka haraka sana na kutumbukia kwenye mtaro wa maji machafu ukajibanza pembeni ya bafu, mlango wa bafuni ulisikika ukijigonga kwa sauti, mume alipofika uani akamuuliza mkewe kuwa "mbona unaoga muda mrefu"? mkewe akamjibu "ndo nimeingia bafuni sa hivi" (kwa sauti ya kutetemeka)
Baada ya kujisaidia mumewe alimulika-mulika huku na kule kwa tochi yake aliyokuwa nayo baadae akarudi ndani, huyu mshikaji anasema amekoma kabisa kumla mke wa jirani yake maana ilikuwa ni chupu chupu akamatwe na alipata michubuko wakati wa vurumai lile.
My take: Mke wa mtu ni hatari, kila mtu atafute wa kwake, sasa hivi vijana wengi hawaoi, wanavizia wake za wenzao tu.