Mbatia akoleza moto wa ESCROW jimbo la vunjo

Dec 21, 2011
71
75



MWENYEKITI mwenza wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), James Mbatia amewataka wananchi katika jimbo la Vunjo mkoani Kilimanjaro, kudai mgao shilingi 609, 000 kwa kila mmoja, toka kwa viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM),fedha zilizotokana na ufisadi katika akaunti ya Tegeta Escrow ya kiasi cha sh,bilioni 321.

Mbatia aliyasema hayo kwa nyakato tofauti katika vijiji vya Mrimbo-Uwo, Matala, Kondiki, Mwika Lole, Maring’a, Msae-Kinyambuo na Kondeni vilivyopo Kata ya Mwika Kusini na Kata ya Mwika Kaskazini, Wilaya ya Moshi wakati akiwanadi wagombea wa nafasi ya Ueneyekiti katika vijiji hivyo.

Mbatia aliyepokelewa katika vijiji hivyo kwa majani ya Masale alisema wananchi hawapaswi kuendelea kuumia kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa maabara na shule za Kata kwa sababu wanao uwezo wa kutumia fedha
zilizochotwa katika akaunti hiyo kuchangia maendeleo.

Source;Mie Mwenyewe.mba
 
ha ha ha. Hii nimeipenda Sana. Ccm Wana Hali ngumu
 
katika utafiti wangu hasa ktk maisha ya kisasa ya kimitandao! taarifa ndani ya JF husomwa au huwafikikia watu wengi zaidi kuliko gazeti lolote lile tanzania/HEKO MBATIA,RUWA AKUTARAME NECHA!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…