Maumivu ya mbavu upande wa kushoto

Maumivu ya mbavu upande wa kushoto

curtis jr2

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2016
Posts
770
Reaction score
4,588
Nitangulize shukrani kwenu nyote wana JF, kwa kazi nzuri ya kuelimishana juu ya mambo mbalimbali katika jamii yetu, Shukrani sana ziwafikie.

Ndugu zangu, Mimi nimekuwa na maumivu ya ndani ya kifua upande wa kushoto ambayo yanaenda mpaka mgongoni, nimekua na tatizo hili yapata miaka mitano(5) sasa, nimekua nikienda hospitalini kufanya vipimo ambapo sijapata majibu sahihi ya kitu kinachonisumbua zaidi naambiwa nina ugonjwa wa Pneumonia na vidonda vya tumbo

Lakini kwangu mimi, maumivu yanakua tofauti nikilalia ubavu Upande wa kushoto ni kama nimechomwa na mshale au kitu chenye ncha kali, ndani hata nikipumua au kuvuta pumzi kwenda ndani naumia.

Naombeni, ushauri nifanye nini au kama kuna mtu aliwahi kupatwa na tatizo kama hili alifanyaje ili kuliepuka

SHUKRANI.
 
Pole sanaa ndugu,
Jitahidi kwenda hospital kubwa kama hukufanya hivyo hapo kabla,

Tunasemaga
"Kikubwa uzima" ila huu usemi tuna utamkaga kimazoea sanaa.
 
Pole sanaa ndugu,
Jitahidi kwenda hospital kubwa kama hukufanya hivyo hapo kabla,

Tunasemaga
"Kikubwa uzima" ila huu usemi tuna utamkaga kimazoea sanaa.
Shukrani sana kaka, ila hosp nmeenda majibu nnayopewa ndo kidogo yanakua magumu kuyaamini,.
 
hapana kaka ila kuna dr mmoja alinambia naweza kuwa na tatizo la Un-balanced Rib
 
1.utakuwa ulishaangukia upande huo
2. Moyo wako umetanuka

Pima xray wqtajuwa kama moyo umetqnuka kuna dawa zake.

Vipi hauna shida ya bp au vichomi?
 
1.utakuwa ulishaangukia upande huo
2. Moyo wako umetanuka

Pima xray wqtajuwa kama moyo umetqnuka kuna dawa zake.

Vipi hauna shida ya bp au vichomi?
mda mwingine napata maumivu kama nachomwa na mshale kwenye ubavu
 
Nitangulize shukrani kwenu nyote wana JF, kwa kazi nzuri ya kuelimishana juu ya mambo mbalimbali katika jamii yetu, Shukrani sana ziwafikie.

Ndugu zangu, Mimi nimekuwa na maumivu ya ndani ya kifua upande wa kushoto ambayo yanaenda mpaka mgongoni, nimekua na tatizo hili yapata miaka mitano(5) sasa, nimekua nikienda hospitalini kufanya vipimo ambapo sijapata majibu sahihi ya kitu kinachonisumbua zaidi naambiwa nina ugonjwa wa Pneumonia na vidonda vya tumbo

Lakini kwangu mimi, maumivu yanakua tofauti nikilalia ubavu Upande wa kushoto ni kama nimechomwa na mshale au kitu chenye ncha kali, ndani hata nikipumua au kuvuta pumzi kwenda ndani naumia.

Naombeni, ushauri nifanye nini au kama kuna mtu aliwahi kupatwa na tatizo kama hili alifanyaje ili kuliepuka

SHUKRANI.
Habari
Kwa maelezo yako bado kunakuwa na mambo mengi sana yanaweza kufikirika kama matatizo kwako kwani ni vyema daktari akaiona sehemu husika, ukifanya nini maumivu hupungua au kuongezeka, dalili nyingine zinazoambatana na hii utapunguza kiasi cha vipimo na magonjwa yanayofikiriwa.

Lakini kwa uchache ninaweza kufikiria:
1: Shida ya moyo
2: Shida ya ngozi inayozunguka moyo
3: Shida ya acid
4: Shida ya ngozi inayozunguka mapafu
5: Shida ya mapafu
6: Shida ya kijiwe kwenye figo
7: Shida ya vivimbe kwenye figo
Ili kupunguza haya ni kama umekutana na faktari na kufanya mahojiano na kuondoa baadhi na baadaye kufanya vipimo.
 
Habari
Kwa maelezo yako bado kunakuwa na mambo mengi sana yanaweza kufikirika kama matatizo kwako kwani ni vyema daktari akaiona sehemu husika, ukifanya nini maumivu hupungua au kuongezeka, dalili nyingine zinazoambatana na hii utapunguza kiasi cha vipimo na magonjwa yanayofikiriwa.

Lakini kwa uchache ninaweza kufikiria:
1: Shida ya moyo
2: Shida ya ngozi inayozunguka moyo
3: Shida ya acid
4: Shida ya ngozi inayozunguka mapafu
5: Shida ya mapafu
6: Shida ya kijiwe kwenye figo
7: Shida ya vivimbe kwenye figo
Ili kupunguza haya ni kama umekutana na faktari na kufanya mahojiano na kuondoa baadhi na baadaye kufanya vipimo.
shukran sani mkuu, hapo kwenye acid ni kweli huwa napata shida sana ya acid na nikeshindwa kula baadhi ya vyakula kwa sababu ya tatizo la acid,.
 
shukran sani mkuu, hapo kwenye acid ni kweli huwa napata shida sana ya acid na nikeshindwa kula baadhi ya vyakula kwa sababu ya tatizo la acid,.

Fika kituo cha afya ili uweze pia kufanya kipimo cha kuangalia wadudu wanaosababisha vidonda vya tumbo kipimwe kwa njia ya choo kikubwa.

Pia, utapewa maelekezo ni nini ule na nini usitumie.

Utapewa dawa ya acid na gasi LAKINI pia bado kutakuwa na haja ya kusikilizwa vyema ili kuhakiki kuwa ni hili pekee au kuna mengine.
Maana tunasema magonjwa hayaongei kuwa kwa kuwa hili lipo basi mengine yasiwepo.
 
Mimi nilikua na tatizo kama lako nilikua nais maumivu ata kupiga miayo nilikua siwezi maumivu yalikua makali sana hasa nikivuta hewa kwenda ndani nilizunguka hospital sana sikupata ata nafuu mwisho nikaambiwa nina Maji kwenye mapafu nikaanzishiwa Dozi ya TB ili kukausha yale maji nashukuru mungu nilipona saivi niko sawa
 
Mi tatizo kama hilo lilinikumba nikiwa o level miaka ya 2000s nilihangaika sikupata dawa nikaachana nalo now naona niko sawa tu. Maana ilikuwa nikivuta pumzi ile kubwa maumivu makali sana.
 
Back
Top Bottom