Salaam kwenu wakuu,
Ninashida moja ya kiafya,kwanza ninahisi maumivu makali kwenye chemba ya moyo,halafu kiungulia kingi na kuna kitu kinanitembea hapa kooni mwashoni mwa koo kuelekea kifuani, yaani kooni Kwa chini, mara kinapotea mara kinakuja na juzi nilikula chakula vizuri tu lakini baada ya Kula kama dk 5 hivi nilihisi maumivu makali Sana chini ya kifua Kwa chini kuelekea tumboni.
Na yakawa yanahama Hama mara chini ya mbavu ya kulia mara chini ya mbavu ya kushoto ila baadae yakapotea ila hiki kitu kilichonikaa hapa shingoni ndo kinanijia mara nyingi hasa nikimaliza Kula naona kinanijia na kiungulia.
Wakuu hili litakuwa ni tatazo gani?