Hello experts, naombeni mchango wenu juu ya hili. Mara nyingi nikiwa na mawazo sana ama kuumizwa na jambo sana huwa napata maumivu makali chini ya ziwa upande wa kushoto.maumivu huwa kama kitu chenye ncha kali na huzidi pale ninapovuta hewa ndani.mara nyingine maumivu husamba mpaka kwenye mkono wa kushoto na mgongoni.kuna kipindi sikuweza kabisa kulalia upande wa kushoto kwani maumivu yalikua yanazidi. Ila nikiwa na furaha na amani bila mawazo hali hii huisha.je ni kitu gani hiki?