Matumizi Aloe Vera!

Sep 27, 2011
19
3
Jf doctor, naomba msaada wako kuhusu matumizi sahihi ya mu aloe vera, mana kuna sites fulani nimezisoma, baadhi zinadai kuwa ni vyema kuitumia aloe vera kwa matumizi ya nje (external use) kwa madai kuwa mu aloe vera unaathari ktk baadhi ya viungo vya ndani ya mwili. Wakati sites zingine zinadai kuwa ni vizuri sana kunywa aloe vera sababu inasaidia kutibu maradhi mengi. Naomba msaada wako ktk hili & nitafarijika kama nitapata na maelekezo sahihi kuhus maandalizi &matumizi! Nawasilisha.
 
mi sio doctor ila aloe vera hata kunywa unaweza ila unatakiwa upate right quantity ukinywa zaidi ni sumu
 
Kwanza ni vema ifahamike kuwa hata hizi dawa za kizungu,nyingi zinatokana na mimea,so inategemeana ile potent ingredient yake ina act wapi.
Katika mwili kuna vitu vinaitwa receptors yaani sehemu maalum ambapo vitu kama dawa au hata vijidudu vya maradhi hujishikiza ili kuweza kufanya kazi. Kwa mfano HIV hujishikiza kwenye receptors maalum zinazopatikana kwenye CD4 za binadamu,hii ni kusema kwamba endapo binadamu atakosa hizi receptors HIV kwake si tatizo maana hawa virus watakosa sehemu ya kujishikiza ili kuleta madhara.

Halikadhalika dawa (potent ingredient) inategemea receptors maalum ambapo itajishikiza ili kuleta effect(faida/madhara).Hizi receptors zaweza kuwa ndani ya mwili(blood vessels,muscles,brain,uterus etc.) au nje ya mwili(skin) lakini pia receptors zaweza kuwa kwenye mdudu ambaye dawa hiyo imelengwa(eg.malaria parasite au hookworm). Hizi receptors ni unique kwa maana kwamba dawa moja inajishikiza kwenye receptor ya pekee kwa namna ambavyo dawa aina nyingine haiwezi kujishikiza pale.Lakini pia receptors zaweza kuwa tofauti kufuatana na mahali zinapopatikana,kwa mfano receptor zilizopo kwenye uterus zaweza kuwa tofauti na za kwenye brain,skin au intestine.Kwa hiyo dawa(potent ingredient) sharti ijishikize(binding) kwenye receptor maalum kwa ajili yake ili iweze kufanya kazi iliyokusudiwa. Otherwise,bila huo uhusiano uliopo (drug/receptor interaction) kazi ya dawa inakuwa hakuna.Kwa kuzingatia maelezo haya,tunaona kwamba upo uwezekano mkubwa kwamba dawa ya kupaka kwenye ngozi isiweze kufanya kazi kwenye brain endapo kanuni ya drug/receptor interaction haitazingatiwa.

Angalizo lingine ni kwamba,ufanyaji kazi wa dawa moja mara nyingi hutofautiana na dawa nyingine na hili huenda likahitaji kwenda ndani zaidi kitabibu ili niweze kueleweka.Lakini pia na namna dawa inavyoyeyushwa katika mifumo ya mwili(body systems) inaamua dawa fulani inafaa kutumika kwa njia ya sindano,vidonge,kupaka au kunusa au vinginevyo.Kwa mfano kuna dawa nyingine huharibiwa ktk mfumo wa umeng'enyaji chakula kabla haijaingia kwenye damu kufanya kazi,hivyo dawa hizi hutolewa kwa njia nyingine kama vile sindano nk.

Sasa tukirudi kwenye issue ya Aloe vera lazima kwanza kuwa na concept hiyo hapo juu.Binafsi sijawahi kutumia product yoyote ya Aloe vera
ila kama inafanya kazi,basi lazima itafuata utaratibu niliouelezea hapo juu.Kusema ni njia gani bora ya kutumia, iwe kupaka, kunywa au vinginevyo si hoja sana;bali itategemea kanuni ileile: potent ingredient/receptor interaction basi! Kwani hiyo ndiyo principle ambavyo dawa hutibu magonjwa.

Ukipata bahati ya kupata jani bichi la Aloe vera,ukiweza kuonja utomvu wake naamini utapata uamuzi kama itafaa kunywa at its raw form au ichakachuliwe kidogo. Zamani akina mama walikuwa wakipaka utomvu wake kwenye chuchu zao ili kuwaachisha watoto wao kunyonya.Binafsi nilimwona mama yangu mzazi akifanya zoezi hili.Kusema kweli utomvu wa Aloe vera unasababisha mtu kujisikia kutapika,na kama utaonja nyingi
kutapika lazima.Nashauri ujitahidi kupata jani lake bichi kisha onja hata kidogo ule utomvi wake,utapata nakala yake bro!

Angalizo,watu unaowaona wanatembeza au kuuza products za Aloe vera wengi ni wamachinga na wafanya biashara tu,kiukweli hawana knowlege ya potent ingredient yake, so ni vema tukanunua na kutumia vitu hivi kwa tahadhari sana.
 
Kwanza ni vema ifahamike kuwa hata hizi dawa za kizungu,nyingi zinatokana na mimea,so inategemeana ile potent ingredient yake ina act wapi.
Katika mwili kuna vitu vinaitwa receptors yaani sehemu maalum ambapo vitu kama dawa au hata vijidudu vya maradhi hujishikiza ili kuweza kufanya kazi. Kwa mfano HIV hujishikiza kwenye receptors maalum zinazopatikana kwenye CD4 za binadamu,hii ni kusema kwamba endapo binadamu atakosa hizi receptors HIV kwake si tatizo maana hawa virus watakosa sehemu ya kujishikiza ili kuleta madhara.

Halikadhalika dawa (potent ingredient) inategemea receptors maalum ambapo itajishikiza ili kuleta effect(faida/madhara).Hizi receptors zaweza kuwa ndani ya mwili(blood vessels,muscles,brain,uterus etc.) au nje ya mwili(skin) lakini pia receptors zaweza kuwa kwenye mdudu ambaye dawa hiyo imelengwa(eg.malaria parasite au hookworm). Hizi receptors ni unique kwa maana kwamba dawa moja inajishikiza kwenye receptor ya pekee kwa namna ambavyo dawa aina nyingine haiwezi kujishikiza pale.Lakini pia receptors zaweza kuwa tofauti kufuatana na mahali zinapopatikana,kwa mfano receptor zilizopo kwenye uterus zaweza kuwa tofauti na za kwenye brain,skin au intestine.Kwa hiyo dawa(potent ingredient) sharti ijishikize(binding) kwenye receptor maalum kwa ajili yake ili iweze kufanya kazi iliyokusudiwa. Otherwise,bila huo uhusiano uliopo (drug/receptor interaction) kazi ya dawa inakuwa hakuna.Kwa kuzingatia maelezo haya,tunaona kwamba upo uwezekano mkubwa kwamba dawa ya kupaka kwenye ngozi isiweze kufanya kazi kwenye brain endapo kanuni ya drug/receptor interaction haitazingatiwa.

Angalizo lingine ni kwamba,ufanyaji kazi wa dawa moja mara nyingi hutofautiana na dawa nyingine na hili huenda likahitaji kwenda ndani zaidi kitabibu ili niweze kueleweka.Lakini pia na namna dawa inavyoyeyushwa katika mifumo ya mwili(body systems) inaamua dawa fulani inafaa kutumika kwa njia ya sindano,vidonge,kupaka au kunusa au vinginevyo.Kwa mfano kuna dawa nyingine huharibiwa ktk mfumo wa umeng'enyaji chakula kabla haijaingia kwenye damu kufanya kazi,hivyo dawa hizi hutolewa kwa njia nyingine kama vile sindano nk.

Sasa tukirudi kwenye issue ya Aloe vera lazima kwanza kuwa na concept hiyo hapo juu.Binafsi sijawahi kutumia product yoyote ya Aloe vera
ila kama inafanya kazi,basi lazima itafuata utaratibu niliouelezea hapo juu.Kusema ni njia gani bora ya kutumia, iwe kupaka, kunywa au vinginevyo si hoja sana;bali itategemea kanuni ileile: potent ingredient/receptor interaction basi! Kwani hiyo ndiyo principle ambavyo dawa hutibu magonjwa.

Ukipata bahati ya kupata jani bichi la Aloe vera,ukiweza kuonja utomvu wake naamini utapata uamuzi kama itafaa kunywa at its raw form au ichakachuliwe kidogo. Zamani akina mama walikuwa wakipaka utomvu wake kwenye chuchu zao ili kuwaachisha watoto wao kunyonya.Binafsi nilimwona mama yangu mzazi akifanya zoezi hili.Kusema kweli utomvu wa Aloe vera unasababisha mtu kujisikia kutapika,na kama utaonja nyingi
kutapika lazima.Nashauri ujitahidi kupata jani lake bichi kisha onja hata kidogo ule utomvi wake,utapata nakala yake bro!

Angalizo,watu unaowaona wanatembeza au kuuza products za Aloe vera wengi ni wamachinga na wafanya biashara tu,kiukweli hawana knowlege ya potent ingredient yake, so ni vema tukanunua na kutumia vitu hivi kwa tahadhari sana.
Ahsante kwa ufafanuzi wako bro, ila tusubiri wenye utaalamu zaidi ktk hili ili watujuze zaidi.
 
Quantity ya kunywa inategemea unataka kutibu ugonjwa gani. Mimi huwa nainywa mara kwa mara kwa ajiri ya colon cleansing. Kama upo interested sema nikuPM namba ya mtaalamu mmoja wa Forever Living akupe maelekezo zaidi
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom