Matokeo ya juhudi za Rais Samia katika uchumi

Matokeo ya juhudi za Rais Samia katika uchumi

Maryam Malya

Senior Member
Joined
Nov 29, 2021
Posts
116
Reaction score
260
Je wajua?

Katika kipindi cha Mwezi Octoba 2022, Serikali chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan imeendelea kufanya vizuri katika maeneo yote muhimu kiuchumi?

MFUMUKO WA BEI- Umeendelea kuwa ndani ya matarajio kwa kiwango cha 5.4%, hii inaifanya Tanzania kuendelea kuwa kati ya nchi chache Duniani zilizoweza kuhimili mtikisiko na kupanda kwa mfumuko wa bei Duniani (Single digit index).

MIKOPO YA MABENKI KWA SEKTA BINAFSI- Ikilinganishwa na Mwezi Octoba Mwaka 2021, Mwaka huu mikopo kwa sekta binafsi imeongezeka kwa asilimia 22, ishara hii ya uhai kwa sekta binafsi inatokana na usimamizi mzuri wa sera na kanuni za kifedha zinazolenga kuimarisha uchumi.

UUZAJI WA BIDHAA NJE YA NCHI- Eneo hili muhimu zaidi katika kukuza uchumi wa nchi yoyote Duniani limeendelea kufanya vizuri zaidi, ambapo uuzaji wa bidhaa umeongezeka kutoka Dola za kimarekani Bilioni 9.4 hadi Bilioni 11.6. Ukuaji huu unachochewa na uongozi imara wa Rais Samia katika kuimarisha Diplomasia na mazingira mazuri ya biashara.

#SisiTumekubali #MamaYukokazini
 
Hali ya uchumi ni mbaya toka tunapata uhuru.
 
Bidhaa zote mhimu ziko juu ya asilimia mia, yaani bei zimeongezeka mara mbili kwa kipindi cha mwaka mmoja afu mfumuko uko single digit? acheni kupika data.
 
Ifike stage tuache uchawa ili taifa lipate maendeleo, WB/IMF imetoa ripoti uchumi wetu umeporomoka kwa kasi, dada unakaa kwenu au umpenga? Unajua bei ya unga, mchele, maharage, mafuta???
 
Back
Top Bottom