Maswali ya Uchaguzi Mkuu.

Maswali ya Uchaguzi Mkuu.

Chivundu

Platinum Member
Joined
Dec 17, 2012
Posts
9,579
Reaction score
13,121
Ndugu zangu,kwanza nawaasa watanzania wa vyama vyote kuilinda amani yetu kama tunu ya Taifa hili.
Pili,naomba tutafakari mambo yafuatayo:
Je,CCM ikishindwa kidemokrasia kabisa,ipo tayari kung'atuka?
Je,UKAWA wakishindwa kidemokrasia kabisa,wapo tayari kukubali matokeo?
Misingi ya maswali haya ni mwenendo wa uchaguzi,chuki iliyokithiri,shauku na mihemko ya pande zote na hofu.
 
Sina hakika kama CCM imeshajiandaa kisaikolojia kushinda na ndiyo maana hata ukiangalia namna wanavyofanya kampeni zake hawafanyi kama wanaogombea ila mgombea wao ameshafanywa Rais mteule na ndiyo maana anatoa matamshi makali dhidi ya wagombea wenzie bila kujua kwamba matamshi yake haya yanaweza kuja kumrudia yeye!
 
Mtu anapokaribia kufa huwapa ndg na jamaa matumaini ya kupona.ccm inaelekea kukata roho.
 
Mimi naweza kusema kwamba uchaguzi huu kwanza tuuweke kwenye maombi yetu ya kila siku, pili wananchi tutambue, tujue na tuelewe maana ya upigaji kura (why people vote?). Tukielewa hilo amani itakuwepo tena bila wasiwasi. Tatizo kubwa linalokumba wale wasiojua maana ya demokrasia wanadhani kuwa kuna ushindi hata kabla ya kupiga kura something which is totally wrong! Hivyo jambo la msingi ni kusubiri kura zikapigwa na tukapokea kitakachotangazwa na mamlaka husika. Wapo wana UKAWA/CCM wanaoona mafuriko ya LOWASSA/MAGUFULI wakadhani ndo ushindi tayari na hao wakitangaziwa kuwa kashindwa ndo wa kwanza kutokubali matokeo hadi machafuko. Wananchi tufute fikira hizo tutambue kwanini watu wapige kura kama mshindi anajulikana? Baada ya hapo tutatulia, rais atapatikana na AMANI ITAKUWEPO. MUNGU IBARIKI TANZANI, MUNGU BARIKI UCHAGUZI.
 
Back
Top Bottom