Habarini wanandugu. Leo nataka kuwafundisha mapishi ya viazi vyakuchemsha. Ni chakula kitamu narahisi sana kupika.
Mahitaji
Viazi mbatata 6
Hoho 2 kubwa
Karoti 3 kubwa
Vitunguu maji 2 vikubwa
Chumvi
Binzari ya simba mbili( curry powder) kijiko kimoja chachakula.
Jinsi yakupika.
Menya viazi navikate nusu (inapendeza ukipata viazi vyaukubwa kidogo).kisha uvioshe vizuri.
Menya vitunguu vikatekate.
Menya karoti, naukate vipande vidogovidogo, katakata. Na hoho vupande vyakiasi.
Chukua sufuria lakiasi, weka viazi na chumvi namafuta yakula kodogo, weka maji ambayo utahakikisha yakikauka viazi vimeiva. Chemsha mpaka maji yakauke na viwe. Vimeiva na kubaki mafuta. Viipuwe. Chukua sufuria lingine mimina yale mafuta yalokua katika viazi weka ule mchanganyiko wako wa vitunguu, hoho, karoti kaanga huku ukiongeza chunvi kidogo nabinzari. Vikishaanza kulainika weka viazi nageuzageuza huku umeweka moto mdogo, baada ya dakika 5 vitakua tear. Ipua naandaa kwakula.
je nikitaka kuweka nazi na ruhusiwa au si ruhusiwi..
Viazi mbatata wengine wanaita viazi ulaya. Nivilaini kuiva hivyo kama unawasiwasi vitakua uji unaweza weka maji kidogokidogo mpaka utapoona vimewiva.sasa mkuu magdarena sisi ambao hatuja wahi kupika hivi viazi mbambata tutajuaje hicho kipimo cha maji huoni ukikosea tu vinakuwa uji mkuu..
mbatata na nazi? Mweh
Viazi mbatata wengine wanaita viazi ulaya. Nivilaini kuiva hivyo kama unawasiwasi vitakua uji unaweza weka maji kidogokidogo mpaka utapoona vimewiva.
Nashukuru kwa somo lako la upishi, aidha bila kupotosha kiswahili hakuna chakula ama viazi vinavyoitwa "viazi mbatata" Kwani kusema hivyo hakuleti maana yoyote ile ni sawa na kusema viazi viazi.Viazi mbatata niviazi vinavyopikiwa chips
Nashukuru kwa somo lako la upishi, aidha bila kupotosha kiswahili hakuna chakula ama viazi vinavyoitwa "viazi mbatata" Kwani kusema hivyo hakuleti maana yoyote ile ni sawa na kusema viazi viazi.
Mbatata ni viazi mviringo/viazi ulaya, na ni jina ambalo limetokana na lugha ya kireno batata lenye maana ya potato. Wakaazi wengi wa pwani na hasa Zanzibar hutumia neno mbatata kumaanisha viazi mviringo/viazi ulaya.