Suala la wanawake kupenda pesa halikuanza leo au Jana, ni la enzi na enzi. Sio hawa wa kileo hata mabibi wa Bibi zetu Ilikuwa ni pesa kwa kwenda mbele. Amini usiamini. Mfano katika jamii za wafugaji mabinti & wanawake wengi walipenda mwanaume shujaa, anaeweza kwenda kuimba ng'ombe na kuzuia ng'ombe wasiibiwe, walipenda waganga wa kienyeji kwani walikuwa ni watu wenye uwezo na walipenda watawala (viongozi wa jadi). Yote haya kwa sababu makundi haya yaliweza kuwahakikishia "usalama & amani" kwani yalionekana ni makundi ya watu shujaa. Ulimwengu wa leo Shujaa ni yule mwenye Pesa, mtu mwenye kuweza kuhakikisha amani na usalama. Wana kosa gani dada, mama na shangazi zetu kupenda wenye pesa. Changamoto kwetu wanaume ni kujituma ili tuweze kuwa na pesa kwani pesa ndio ushujaa, kinyume chake tutaishia kupata "reject".