Kuna watu wa ajabu sana dunia hii. Yaani hata kwenye tatizo kubwa lenye kuhuzunisha unakuta mtu anatumia fursa hiyo kufanya ufuska wake. Mtu anaaga anakwenda msibani na kweli anafika ila anazuga dakika chache ili aonekane alikuwepo halafu anatokomea kwenye ngono. Huu ni ushenzi uliopitiliza.
Hi iliwahi kumtokea jirani yangu mkewe alikuwa mwepesi sana kuhudhuria misiba hata isiyomhusu tena ile ya mbali kumbe anaenda kukamilisha ufuska wake lakini za mwizi ni arobaini akabambwa kilaini baada ya mume kutonywa na kufatilia kimyakimya. Kilichofuta ni talaka maana ni ngumu kuishi tena na kahaba wa aina hii.
Yaani kuna mijitu ngono zimetawala akili zao, alistahili kabisa hiyo talaka maana this is too much,. Nasema tumechoka, tumechoka nasema na wachwe tu maana...!!!!