Mapenzi kizunguzungu, kihindihindi, kiafrika afrika, kiarabuarabu, mwisho naona kizungumkuti

bigmind

JF-Expert Member
Oct 28, 2015
12,457
12,668
Jamaaaani haya mapenzi kwanini yasiwe na formula basi tukajua kama nikwenda kuyasomea kuzama darasani ikajulikana moja.

Mpaka sasa natamani mapenzi ya kweli bora yangekuwa yanauzwa supermarket ningefanya kazi kama punda ili siku moja nipate pesa kiasi cha kutosha kuyanunua ili niyafurahie angalau...!

Najua unasoma midomo iko wazi ukicheka kwa kufurahia au kuvuta umakini kwa haya maneno ya kwenye hii habari ila ninayeandika hapa nagugumia maumivu ya hatari sana.

Sikwamba nimeachwa ila iko hivi kwanini mara nyingi hisia kati ya wakaka na dada hazijabalance jamani, mwenzenu nina warembo wanne sasa zoezi la kuchagua nani awe mke limekuwa gumu sana, kati ya hao warembo wanne yupo dokta,mwalimu, mhifadhi na hotelia ila binafsi nawapenda wawili ambao ni mhifadhi na hotelia kwa mapenzi sawa kabisa kiasi kwamba ata watake niwaoe wote sitaona shida.

Sasa songombindo iko hivi hawa wapendwao ndiyo kabisa upendo wao kwangu kiduchu sana. Teacher na dokta wamejifia kabisa hawajiwezi tena ila ndiyo hivyo sina time nao, huwa nawaweka guard mpaka nawahurumia.

Ushauri ninao wapenda hawanipendi nisio wapenda nawalaza macho wakinipetipeti...!

Sina nia mbaya msije nishambulia nimechanganyikiwa hapa.
 
Drive formula yako mwenyewe tuu mkuu manake kusubiri mpaka mgunduzi azaliwe co leo... fanya maamuzi magumu
 
Wewe tu hujajua kuyabalance hapo.....
Wanawake wanne wote na bado unalia? Ungekua na mmoja roho yako ingeacha mwili....
Kiaje sasa unajua ili ufanye uchaguzi lazima wawepo unao wachagua sasa hapo ndo nimechanganyikiwa mwenzenu...
 
Kwakua una uzoefu katika kuchepuka Hapo kazi ndogo mkuu. Muoe usie mpeda hapo hasa huyo doctor.alafu hotelia muweke mchepuko.

Hapo hutowaza kwakua doctor ratiba zake hazieleweki mara mchana mara usiku hapo wewe utakua unapata muda wa kuchepuka na hotelia hasa usiku si huo muda hafanyi kazi. Hapo hutojutia

Baada ya hapo ni pm namba ya teacher nina machache ya kuzungumza nae
 
Kwakua una uzoefu katika kuchepuka Hapo kazi ndogo mkuu. Muoe usie mpeda hapo hasa huyo doctor.alafu hotelia muweke mchepuko.

Hapo hutowaza kwakua doctor ratiba zake hazieleweki mara mchana mara usiku hapo wewe utakua unapata muda wa kuchepuka na hotelia hasa usiku si huo muda hafanyi kazi. Hapo hutojutia

Baada ya hapo ni pm namba ya teacher nina machache ya kuzungumza nae
Ushauri wako hapana nataka nitulie ndoani aisei good father/dad..
 
Kwakua una uzoefu katika kuchepuka Hapo kazi ndogo mkuu. Muoe usie mpeda hapo hasa huyo doctor.alafu hotelia muweke mchepuko.

Hapo hutowaza kwakua doctor ratiba zake hazieleweki mara mchana mara usiku hapo wewe utakua unapata muda wa kuchepuka na hotelia hasa usiku si huo muda hafanyi kazi. Hapo hutojutia

Baada ya hapo ni pm namba ya teacher nina machache ya kuzungumza nae
safi sana fursa popote
 
Ushauri wako hapana nataka nitulie ndoani aisei good father/dad..
Hapo utatulia automatically. Kwakua doctor anakupenda akikufuma atakuaa anakusamehe na atabaki anakupenda tu. Na huyo hotelia akisikia umeoa atakua ana kisirani sana na wewe ila hatokuacha kwakua atataka kukuchuna. Na wewe baada ya kuchunwa sana moyo utapunguza upendo na upendo uliopungua utahamia kwa mkeo, mwisho wa siku utajikuta unampenda sana mkeo.

Mkuu suala la no ya ticha naona haupo makin nalo
 
Kwanza umelishushia hadhi jina lako.
Pili unaowapenda hawakupendi na usiowapenda kivile ndo wanakupenda khaswa hiyo ndio fomula ya mapenzi ilivyo ni wachache sana unakuta wame match ila wengi huzugana so funga nafsi oa acha kuchezea mioyo ya watoto wa mwanaume mwenzetu.
 
Hapo utatulia automatically. Kwakua doctor anakupenda akikufuma atakuaa anakusamehe na atabaki anakupenda tu. Na huyo hotelia akisikia umeoa atakua ana kisirani sana na wewe ila hatokuacha kwakua atataka kukuchuna. Na wewe baada ya kuchunwa sana moyo utapunguza upendo na upendo uliopungua utahamia kwa mkeo, mwisho wa siku utajikuta unampenda sana mkeo.

Mkuu suala la no ya ticha naona haupo makin nalo
Mmmhh! Natamani haya yatokee mara moja n iachane na hii kadhia...!
 
Wanawake wanne hujui uchague yupi, una wanawake au una mawe?
Hujaambiwa ninatekeleza moyo unachonituma ila ndiyo hapo changamoto ndogondogo uneyempenda hakupendi kiivyo usiyempenda usiku kucha anakulilia
 
Kwanza umelishushia hadhi jina lako.
Pili unaowapenda hawakupendi na usiowapenda kivile ndo wanakupenda khaswa hiyo ndio fomula ya mapenzi ilivyo ni wachache sana unakuta wame match ila wengi huzugana so funga nafsi oa acha kuchezea mioyo ya watoto wa mwanaume mwenzetu.
Mkuu siyo suala dogo la kuletea mzaa bora upotee njia utauliza siyo upotee kuoa..! Utatamani ndoa ya jirani yako.
 
Back
Top Bottom