Inawezakana tangu mwanzo ulikuwa na mtazamo usio sahihi wa mapenzi na ndiyo maana ukajikuta umekuwa na mademu wengi ukifikiri kila mpya utakaye mpata anaweza kukufanya ufurahie mapenzi na mwisho wa siku adhma yako haikutimia. Ukweli ni kuwa, mapenzi ni zaidi ya kutafuta mademu au kumuacha wa zamani na kuwa mapya. Mapenzi yanajumuisha social life, upendo wa dhat, kushirikishana, kuthaminiana, kusaidiana, maongezi mema nk. Pia ni suala la kisaikolojia. Jaribu kukaa na huyo uliyenaye sasa, kuwa karibu naye, toka naye, ongea naye, furahi naye, shirikianeni nk utaona matunda yake.