Maoni kuhusu Magereza

Masalu Jacob

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2017
Posts
1,341
Reaction score
1,498
Napenda kuishauri Serikali kwasasa kuhusu huduma katika magereza kuanzia usafi, afya za wafungwa, mavazi nadhifu, mahala pa kulala na haki ya kupata taarifa.

Mapendekezo:
1. Je, Serikali haioni kuna umuhimu sasa Magereza yaboreshwe na kujengwa kwa mtindo wa hostel za kisasa.

2. Je, Serikali kwanini isianzishe mfumo mzuri wa huduma ya chakula kwa wafungwa kula vyakula vizuri tena iwe milo hata 3 kwa kutwa.

3. Magereza yote nchini yawe na mazingira mazuri ya kupumzika kwa wafungwa wawe na uwezo wa kupunga upepo na kurefresh akili.

4. Mfungwa/ wafungwa wapate haki ya habari kuhusu nchi yao na pia kuwe na mfumo mzuri wezeshi wa kushirikishwa maendeleo yaliyopo mtaa au kijiji wanachotoka.

Karibu.
 
Ni kweli ila mfungwa AFRIKA ni kama mtumwa enzi za UKOLONI!.
Hivyo kuna umuhimu wa kuliangalia hilo.
 
Hivi huwa wanakula milo mingapi kwa siku?
 
 
wafungwa wanatakiwa kupigwa mateke na kula mara moja kwa siku, haiwezekani wafanye fujo alafu wakaishi vizuri kuliko sie tuliomaliza vyuo vikuu na kukosa ajira
 
Hivi kwanini jela wafungwa wasiwe wanaruhusiwa kupiga simu atleat Mara moja.kwa mwezi.
 
ahaa kuna watumishi wa umma hawapati hizi facillities alafu wafungwa ndo wapate,
Inawezekana ila bado kwanza,tena bado sana,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…