Toosweet
JF-Expert Member
- May 27, 2012
- 2,140
- 1,982
Kwenu,
Inapotokea mbunge au diwani amefariki tunafanya uchaguzi wa marudio. Hii ni gharama ambayo pengine haina bajeti.
Kwa upande mwingine, akitokea mbunge au diwani 'ameenda kumuunga mkono' Rais Magufuli kwa kukimbilia CCM, tunafanya uchaguzi pia.
Hivi kuna lazima gani kuitisha uchaguzi mdogo ambao kwa kawaida hugharimu fedha na maisha ya watu na hasa wanachama na viongozi wa upinzani? Sijawahi kuona au kusikia mtu yeyote anayemuua mwanachama na kiongozi wa upinzani akikamatwa.
Mauaji na utekaji hufanywa kwa kupangwa lakini wahusika hawakamatwi. Wanaokamatwa ni upande wa wanaouawa. Sasa tuna raia first class na wengine third class. First class hawakamatwi wala kufungwa
Serikali ilete muswada au marekebisho ya sheria ili mbunge au diwani kutoka chama chochote akihama chama wakati bado anahudumu, aapishwe mbunge au diwani aliyefuatia kwa wingi wa kura na kusiwe na haja ya marudio ya uchaguzi.
Tabia zinazoendelea kwa sasa za hama hama, zinasababisha wapigakura kutokuona umuhimu wa kupiga kura.
Ni mawazo yangu tu.
Inapotokea mbunge au diwani amefariki tunafanya uchaguzi wa marudio. Hii ni gharama ambayo pengine haina bajeti.
Kwa upande mwingine, akitokea mbunge au diwani 'ameenda kumuunga mkono' Rais Magufuli kwa kukimbilia CCM, tunafanya uchaguzi pia.
Hivi kuna lazima gani kuitisha uchaguzi mdogo ambao kwa kawaida hugharimu fedha na maisha ya watu na hasa wanachama na viongozi wa upinzani? Sijawahi kuona au kusikia mtu yeyote anayemuua mwanachama na kiongozi wa upinzani akikamatwa.
Mauaji na utekaji hufanywa kwa kupangwa lakini wahusika hawakamatwi. Wanaokamatwa ni upande wa wanaouawa. Sasa tuna raia first class na wengine third class. First class hawakamatwi wala kufungwa
Serikali ilete muswada au marekebisho ya sheria ili mbunge au diwani kutoka chama chochote akihama chama wakati bado anahudumu, aapishwe mbunge au diwani aliyefuatia kwa wingi wa kura na kusiwe na haja ya marudio ya uchaguzi.
Tabia zinazoendelea kwa sasa za hama hama, zinasababisha wapigakura kutokuona umuhimu wa kupiga kura.
Ni mawazo yangu tu.