R.B
JF-Expert Member
- May 10, 2012
- 6,296
- 2,578
Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad, akimpongeza Mhe. Mansour Yussuf Himid baada ya kuamua kujiunga na chama hicho na kumkabidhi rasmi kadi ya CUF katika viwanja vya Paje, Wilaya ya Kusini Unguja.
Mansour alikua Mwakilishi wa Kiembesamaki Kabla ya kuvuliwa Uwakilishi na CCM. Mwaka 2000 hadi mwaka 2004, alikuwa Naibu Waziri wa Maji, Ujenzi, Nishati na Ardhi, na kati ya mwaka 2004 hadi mwaka 2010 alikuwa waziri kamili katika wizara hiyo na baadaye mwaka 2010 hadi mwaka 2012, alikuwa Waziri wa Kilimo na Rasilimali. Kwa habari zaidi kumuhusu, soma=> CCM yamvua uanachama Mwakilishi wa Kiembesamaki, Mansoor Yussuf Himid