Maneno ya hekima ya kutafakari

wa stendi

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2016
Posts
26,008
Reaction score
28,342
*Nyati wanaua watu 7 kila mwaka.*
*Simba wanaua watu 500 kila mwaka.*
*Kiboko wanaua watu 800 kila mwaka.*
*Mabuibui wanaua watu 5000 kila mwaka.*
*Nnge wanaua watu 7000 kila mwaka.*
*Nyoka wanaua watu 10000 kila mwaka.*

*Kisha cha kushangaza,*

*Mbu wanaua watu milioni 2.7 kila mwaka...! Ndio... Walio wadogo kabisa ndio wanaoua sana..!!*

*Dhambi ndogo ndogo, ambazo wengi hawazioni au hawazitambui, ndio zenye kuua zaidi maisha yako ya kiroho (imani).*

*Epuka kutosali kutenga muda mchache wa siku yako kwa ajili ya Mungu wako.*

*Dhambi za upungufu zinaua kama dhambi za uamuzi tu..!*

*Kusengenya na uongo mdogo mdogo, kunafanywa mara kwa mara na ndio mauti.*

*Chunga yale madogo madogo unayoyafanya kila siku, ndio yatakayo kuangusha.*

*Watu wa kufanikiwa wana mambo mawili midomoni mwao: _Tabasamu na Kimya_.*

*Tabasamu inaweza kutatua matatizo, na kimya kinaweza kuepusha matatizo.*

*Sukari inaweza kuchanganywa na chumvi, lakini siafu wanaikataa chumvi na wanaibeba sukari pekee.*

*Chagua watu wa sawa katika maisha, uyafanye maisha yako yawe bora na matamu.*

*Ukishindwa kufikia ndoto zako, badilisha mbinu wala sio Mungu wako*

*Kumbuka miti hubadilisha majani yake, wala sio mizizi yake.*

*Hutafikia unakokwenda (lengo lako) ikiwa utasimama kurushia mawe kila mbwa anaye kubwekea.*

*Wapinzani wakikuona unatembea kwenye maji, watasema ni kwasababu huwezi kuogelea.*

*Hata ukicheza kwenye maji, maadui wako watalalamika unarusha vumbi.*

*Fanya hamu yako iwe kuishi maisha ya utulivu, kutizama yako, na kufanya kazi kwa mikono yako.*

*Kumbuka usishindane hata na nguruwe... Mutachafuka nyote lakini nguruwe atafurahia..!*


*KUWA MWENYE HEKIMA*
Kosa mahali popote ila kwa Mungu usikose.

Tafadhali usidharau dhambi ndogo ndogo ili tuuone ufalme wa mbinguni
 
Hii elimu niliikosa darasani nakuja kuipata mtaani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…