Mamlaka ya Maji Safi na Maji taka Morogoro (MOROWASA), mnatutesa na maji machafu wananchi

Uncle Jei Jei

JF-Expert Member
Jan 7, 2011
1,684
2,157
Hii ni kero kubwa hapa Morogoro mjini. Kwa takribani mwezi mmoja sasa sisi wakazi wa Morogoro majumbani mwetu tunapata maji machafu na yenye harufu kali mithili ya maji ya kwenye chemba za chooni!!

Hali hii inasikitisha sana. Na kibaya zaidi swala hili limechukua muda mrefu sana kinyume na matumaini tuliyopewa na baadhi ya wafanyakazi wa idara hiyo tulipo hoji mwanzoni kabisa

Tunaomba idara na mamlaka husika mlimulike swala hili kwa uzito kwani sisi wakaazi wa Manispaa hususani mitaa ya Mafiga na Misufini tunateseka sana!

Haya maji hayafai kwa matumizi ya binadamu lakini kwa sababu ya shida na kukosa mbadala tunalazimika kuyatumia hivyo hivyo kwa kutegemea kudra za mwenyezi Mungu kitu ambacho ni cha hatari sana tena sana.

Nisisi wakaazi wa Morogoro kutoka mitaa ya Mafiga na Misufini, tunaomba vyombo vya habari mtusaidie kupaza sauti kwa hili ili wahusika watuondolee kero hii kwani sisi tumeongea hadi tumechoka
 
Watu wa moro wanavumilia tu moro maji yake machafu sana typhoid nje nje

Halafu wanavyojua kukata maji khaaa

Idara ya maji moro imeoza kitambo sana basi tu
 
Kwa kweli maji ya Moro ni komesha kwa uchafu na kunuka khaa; kunawa tu uso unajifikiria, ndo uwaze kuyatumia kwa matumizi mengine. Nyumba hadi inanuka kisa maji seeeee. Too much

C.c espy mito
 
Kwa kweli maji ya Moro ni komesha kwa uchafu na kunuka khaa; kunawa tu uso unajifikiria, ndo uwaze kuyatumia kwa matumizi mengine. Nyumba hadi inanuka kisa maji seeeee. Too much
Halafu sasa na sisi tulivyowaajabu bado kila mwezi tunalipa bili ya maji! Yaani sijui tumerogwa!!? Binafsi nimegombana na Mother house kwenye kulipia maji yanayonuka nilivyoona ugomvi sio wake kwani anaogopa gharama za kuyarudisha endapo watayakata, nikaamua kwenda idara husika, dah! Majibu niliyopewa unaweza kurusha ngumi!
 
Halafu sasa na sisi tulivyowaajabu bado kila mwezi tunalipa bili ya maji! Yaani sijui tumerogwa!!? Binafsi nimegombana na Mother house kwenye kulipia maji yanayonuka nilivyoona ugomvi sio wake kwani anaogopa gharama za kuyarudisha endapo watayakata, nikaamua kwenda idara husika, dah! Majibu niliyopewa unaweza kurusha ngumi!
Hivyo vi maji vyenyewe vinavyotoka sasa, kama ndo unakinga ndoo moja moja basi kwa hiyo speed siku nzima unaweza kuitumia kukinga maji tu. Kama unatumia Tank subiri siku yamepungua hehe hukawii kukuta umeshakuza na vyura humo. Maji unaona kabisa vijidudu mara sijui uchafu gani + harufu hiyo ptuuuu. Moruwasa wametuchoka aisee. Walikwambiaje?
 
Hii ni kero kubwa hapa Morogoro mjini. Kwa takribani mwezi mmoja sasa sisi wakazi wa Morogoro majumbani mwetu tunapata maji machafu na yenye harufu kali mithili ya maji ya kwenye chemba za chooni!!

Hali hii inasikitisha sana. Na kibaya zaidi swala hili limechukua muda mrefu sana kinyume na matumaini tuliyopewa na baadhi ya wafanyakazi wa idara hiyo tulipo hoji mwanzoni kabisa

Tunaomba idara na mamlaka husika mlimulike swala hili kwa uzito kwani sisi wakaazi wa Manispaa hususani mitaa ya Mafiga na Misufini tunateseka sana!

Haya maji hayafai kwa matumizi ya binadamu lakini kwa sababu ya shida na kukosa mbadala tunalazimika kuyatumia hivyo hivyo kwa kutegemea kudra za mwenyezi Mungu kitu ambacho ni cha hatari sana tena sana.

Nisisi wakaazi wa Morogoro kutoka mitaa ya Mafiga na Misufini, tunaomba vyombo vya habari mtusaidie kupaza sauti kwa hili ili wahusika watuondolee kero hii kwani sisi tumeongea hadi tumechoka
Uncle Jei jei mimi nawaonea huruma dada zetu wanayotumia haya maji kunuka kuoshe papuchi zao,UTI itawamaliza.
 
Uncle Jei jei mimi nawaonea huruma dada zetu wanayotumia haya maji kunuka kuoshe papuchi zao,UTI itawamaliza.
Mbali na dada zetu pia kuna watoto. Kifupi haya maji hayafai kabisa! Yaani ukiyaweka ndani yanatoa harufu utadhani chemba za choo zimejaa sasa zinatema nje
 
Sidhani kama hiyo Mamlaka ina kiongozi hadi sasa, kuna mabomba mengi yamepasuka mtaani yanamwaga maji hovyo, ukiwapa taarifa kuwa maji yanapotea hovyo wakati watu wengine hawana maji, they take no action
 
Kwa kweli maji ya Moro ni komesha kwa uchafu na kunuka khaa; kunawa tu uso unajifikiria, ndo uwaze kuyatumia kwa matumizi mengine. Nyumba hadi inanuka kisa maji seeeee. Too much

C.c espy mito
Vumilia tu dota, sie watanzania tu wapole na wavumilivu sana, ndio maana hautuna furaha, hata Sudan inatushinda
 
Mbali na dada zetu pia kuna watoto. Kifupi haya maji hayafai kabisa! Yaani ukiyaweka ndani yanatoa harufu utadhani chemba za choo zimejaa sasa zinatema nje
Ole wako ukute unayaifadhi kny zile chupa/vidumu vya uhai vya 12lts hiyo harufu ni balaa.
 
Tafadhali, mliokaribu na vyombo vya habari hasa magazeti, redio na ikiwezekana Television tufikishiieni hii kero hewani huenda wahusika wakajirekebisha au basi kuchukuliwa hatua.

Naamimi humu kuna waandishi wa habari na wafanyakazi wa vyombo vya habari mbali mbali. Nyie mna nguvu kubwa ya kutusaidia kwa hili.
 
Vumilia tu dota, sie watanzania tu wapole na wavumilivu sana, ndio maana hautuna furaha, hata Somalia inatushinda
Mmh too much aisee. Sasa Yale maji unayatumia kufanyaje kama tu usafi wa nyumba utanukisha nyumba
 
Mmh yaani baada ya miez nane maji ndo yametoka Leo halafu machafuu

Morowasa jirekebisheni
 
yani hii thread ilikuwa akilini mwangu.nina wiki 2 morogoro nimeona hii hali najiuliza wakazi wake wanaridhika au ndo waoga.wanakera sana hawa watu, maji yenyewe yanatoka kwa mahesabu yakitoka yanakuwa na rangi ya ajabu kwa ufupi huwezi yatumia kupikia au kunywa.
 
Back
Top Bottom