Umenikumbusha one time kuna huyu binti kwenye basi la mkoa alileta huu uswahili. Amepanda kwenye basi amevaa jeans, sweater, na kablouse. Basi hana hata pochi yaani yupo kisela sana.
Kilichotokea ni period ilimuanza ghafla bila kujua. Kilichofanya nijue ni alivua sweater lake na kulitumia kama kujifunika sasa mimi nilikuwa na sweater na zile shuka za kimasai. Nikamuuliza mbona umevua sweeter na gari wamewasha AC haikutesi?!
Akajibu kama vile mtu mwenye mawazo na aibu fulani. Ilinichukua dakika chache kunotice kuwa hakuwa sawa na nikashajua huyu ametumia sweater kujificha. Nikamwambia kwa sauti ya chini sana unahitaji msaada. Hakunijibu zaidi ya kuinama kama anaona aibu halafu anaweka lile tabasamu la aibu fulani.
Nikamwambia niandikie kwenye sms unataka msaada gani. Nikampa simu yangu aandike namba yake nikamtext akaanza kuchat akanambia ameingia Period hapo hana uhakika na kinachoendelea ila anahisi amechafua siti sasa hajui pa kuanzia.
Aiseee ni MUNGU tu alisimamia ile situation maana gari lilikuwa na utingo mwanaume tu. So ikabidi nimfuate nimpange kuwa atusaidie wakiona hata kituo cha mafuta wasimame konda akanielewa. Tukasimama akasema abiria tuchimbe dawa kidogo. Watu wakaanza shuka. Akachukua sweta akaliweka pale kwenye siti halafu nikampa shuka langu la kimasai akajifunika mwili mzima so muda tunatoka nashuka nae hakuna mtu alishtukia chochote hadi tunafika chini. Nikamwambia atangulie chini me nakwenda tafuta pedi. Nikaenda mnunulia duka liko huko barabarani kipande kidogo toka pale kwenye sheri nikamletea.
Akajiweka sawa suruali yake ilikuwa imechafuka akaisuuza na maji akavaa hivyo hivyo nikamwambia valia na hilo shuka la kimasai. Tukarejea kwenye gari. Aisee ikawa kama ni mke wangu sasa namna tulivyorudi na kukaa kwenye gari alijiegemesha kwenye kioo me namwambia niegemee kama unataka kulala.
Tulishuka sote stand ya Moshi alikuwa anataka kwenda nikamwambia sidhani kama utakuwa katika hali nzuri kuendelea na safari katika hali hiyo na muda umekwenda twende nyumbani sio mbali na hapa ukaweke mambo sawa uwe safi kesho utaendelea na safari ndugu zako waelezee situation wakitaka watumie picha kabisa halafu tukimbie na huu msala wa kuchafua siti.
Akakubali. Tulishuka sote akafika nyumbani akatoa nguo zote akazifua na kuzianika. Ilibidi nimnunulie kufuri mpya na pedi zingine za brand nzuri.
Nilimpa risala sana ule usiku. Kwamba kwann mtoto wa kike unasafiri kirahisi vile huoni namna umejihatarisha. Yaani unasafiri haubebi kitenge hata viwili na hata pedi tatu za dharula maana hata usipopata wewe anaweza pata mwanamke mwenzako ukamsitiri. Nikamwambia sasa usingekutana na mimi leo si ungefedheheka sana.
Kesho yake nikamsindikiza jioni aende kwa kwao huko Arusha. Na baada ya hapo tuliendelea kuwasiliana she is someone very close to me now.
Hii inanikera sana na mwanga unaumiza.Mwanga wa simu nyakati za usiku! Unakuta jirani yako akiwasha simu gari zima mnaonana
Ukisafiri jaribu hata kuweka simu vibration au punguza mlio
Usiombe ukae na mtu simu ikiita ina mlio singeli si singeli,bongo fleva si bongo fleva yani haieleweki alafu mlio mkubwa utasema masikio yake yameziba hasikii mlio mdogo!
Yani kila simu ikiita ulieko pembeni lazima ustuke,hii inaboa sana!
Yani ndio Bus linatoka mule Mbezi Louis kuitafuta Morogoro road, mama na mtoto waliokaa pembeni yangu wote kwa pamoja wakaanza kutapika. Dakika sifuri tu nimepakwa matapishi dadek.
Sijawahi kusafiri kwa raha mimi.
Enzi za Mohammed trans, natoka kanda ya ziwa kuitafuta Dar. Kuna wabibi ndani ya bus wanasafiri na wajukuu wao wadogo sana kiumri. Mmoja kati yao akaachia uharo kwenye corridor zile za katikati ya siti. Bus zima tulitafutana kwa hiyo harufu yake!
Mara nyingine tena natoka Dar kwenda Kanda ya Ziwa, ndani kuna familia ya hawa ndugu zetu wasukuma. Yani mmoja amekaa siti ya nyuma kabisa, anapiga story na mwenzie aliekaa siti ya katikati ya Bus. Walipanda na ndoo ndogo ya maji ya kunywa, wanachota kwa kikombe then wanapasiana kutoka nyuma mpaka katikati. Siku hiyo kabila lote la wasukuma lilinikwaza!
Mara ya mwisho nimepanda Bus, siti ya pembeni akakaa mzee mmoja hivi. Asee mzee alikua ananuka tumbaku sijawahi ona. Kila watu wakishuka kula na kuchimba dawa, yeye anashuka kuvuta tumbaku zake. Nilifika kwa tabu sana wakuu!
Anataka msikilizie mdundo,utajua hujui nakwambiaNa ikiwa inaita hapokei anaiacha kidogo ichanganye mpate ladha [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Kulikuwa hamna kimasihara kwel apo[emoji3][emoji3]Siku iyo niko Moro msamvu mida ya saa 4 usiku Nasubiri usafiri wa kwenda Dar ikaingia New Force ya kutoka Sumbawanga ilijaa ila nikapanda ivyoivyo, sasa nikawa nimesimama.
Sasa karibu na kwenye siti niliosimama kulikuwa na mkaka anachati na mke wake, mke wake akawa anamwambia mumewe umeme nyumbani kwao umekatika, basi mwanaume akamjibu, kwahiyo leo tunatom**na kwenye giza?!! Nikashindwa kuvumilia nikacheka yule kaka akanigeukia tukaaangaliana wote tukaanza kucheka teena [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Siku iyo niko Moro msamvu mida ya saa 4 usiku Nasubiri usafiri wa kwenda Dar ikaingia New Force ya kutoka Sumbawanga ilijaa ila nikapanda ivyoivyo, sasa nikawa nimesimama.
Sasa karibu na kwenye siti niliosimama kulikuwa na mkaka anachati na mke wake, mke wake akawa anamwambia mumewe umeme nyumbani kwao umekatika, basi mwanaume akamjibu, kwahiyo leo tunatom**na kwenye giza?!! Nikashindwa kuvumilia nikacheka yule kaka akanigeukia tukaaangaliana wote tukaanza kucheka teena [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Kaliwa tayariAlaf ikawaje sasa
Kaliwa tayari
[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2]Hii ilinikuta uswahilini, niliwapita wakaazi , nilipotelea chochoro, nikatokezea bafuni
Nilivyorudi kuuliza njia nkikaambiwa tulidhani unaenda kuoga tulikuwa tunajadili wa kukuletea maji
Alaf ikawaje sasa
Kaliwa tayari
Si tukaishia kucheka akaniambia wee chaumbea njoo ukae nikakaa yeye akanipokea kusimama, Mikese kuna abiria akashuka wa siti nyingine akakaa, sijui waliongea nini na konda nashangaa konda ananiambia sister hamia siti ya uku mpishe huyu akae sijui walimshawishi nini mpaka akakubali, nikamgomea konda sirudi nyuma [emoji23][emoji23]
Konda akasema dada utakosa mume wa kukuoa wewe! Ghafla yule bwana si akaja eti njoo yuko serious as if me mkewe, nikamwambia sitaki akasema toka kwenye siti yangu nikae, na mimi nilivyo jeuri nikanyanyuka nikaenda ile siti iliyokuwa wazi nikakaa akamwambia yule abiria aliyemtoa ile siti eti njoo ukae jamaa yangu! Akanifata nilipokaa akakaa nikajinyamazia zangu kimya!
Akaniambia kwanini ulikuwa unasoma msg zangu?! Nikanyamaza akaniambia, unajifanya mstaarabu kumbe mpenda chabo sasa twende ukamalizie kutushikia tochi ilibidi tu nicheke [emoji23][emoji23]
Jamaa ni mtu wa utani mwingi ikabidi niwe mpole niendelee kucheka na jamaa ana vituko na story za uongo! Alikuja kuniteka alivyoleta story za siasa ndio nazipenda basi tukajadili mpaka safari ikawa fupi.
Nikaja kugundua jamaa ni mfanyabiashara maeneo ya nyanda za juu kusini na alinisaidia sana kunifundisha biashara ila ilichukua muda sababu sikuwa na ilo wazo before! Mpaka leo amekuwa mtu wangu wa karibu sana!
Kwani kila atakaekuomba no au kukutongoza lazima umkubalie bibie?,ukiwa kama mwanamke kutongozwa ni lazima ila ni utashi wako kuamua kukubali ama kukataaHii naomba iwe namba moja [emoji23][emoji23][emoji23]