Teknolojia ni Yetu sote
JF-Expert Member
- Apr 28, 2020
- 1,221
- 2,425
Baada ya Infinix kutangaza toleo jipya la simu zao ambayo ni Infinix Note 50 Series' , kwa kweli wameboresha mambo mengi sana kwenye hii toleo jipya kikubwa zaidi ni kuhusu ujio mpya wa AKILI bandia inayokusaidia kufanya mambo Mbalimbali kwa haraka na urahisi.
๐ก Kioo chake ni chembamba
Hii simu imekuja ikiwa na AMOLED flat display yenye inchi 6.7 ikiwa na muundo wa STB skrini to body ni nyembamba wallah , inapendeza machoni mwa watu ukishika una enjoy pamoja na kutumia refresh rate yake ni 144Hz iko very smoothly.
๐ Battery ni Super
Battery lake ni 5200mah ndani ya dakika 30 utaweza kuchaji simu yako na kujaa faster ikiwa na 90W + fast charger 3.0 support. Pia unaweza chaji simu yako kwa mfumo wa wireless kwa kukuletea Mag Pad Wireless charging pad yenye 20W.
๐ธ Camera
Hii simu kamera yake ni nzuri mnoo asikuambie mtu aiseeh, inatoa picha nzuri za kuvutia unaweza sema umetumia kamera mbugani. Ina 50mp ikiwa na sensor ya Samsung ya ISOCELL GN 5 inayotoa picha Kali balaa.
Nakuambia tena picha zake ni Kali balaaa๐ธ.
๐ก Infinix Ai
Kwa kweli kwenye Ai siwezi kuwadai Chochote kwa hapa wametisha kwanza Wana Ai Eraser yenye uwezo wa kuondoa kitu usichotaka kwenye picha yako bila kuharibu uhalisia wa picha tofauti na AKILI bandia ya Apple kwenye iphone.
Utaweza ku double tap kwenye batani ya pendeni utaweza kumuwasha AI anaitwa Folax akiwa na muingiliano na Deepseek Chochote unachomuuliza basi anakusaidia chap bila shida yoyote.
โก Processor yake
Imekuja ikiwa na Processor yenye nguvu MediaTek Helio G100 ultimate yenye uwezo wa kucheza game yoyote bila kuganda Ganda, kuanzia call of duty, Bright memory infinity yani simu kupata Joto sahau, Wala kuisha chaji unatumia bila wasiwasi.