Mama Wema Sepetu na kauli za Edward Lowassa!

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,171
23,996
Lowassa aliingia CHADEMA kwa usanii wa kuja na wabunge 50 wa CCM, wenyeviti wa mikoa wa CCM zaidi ya 22, Wenyeviti wa wilaya zaidi ya 80 na wakuu wa wilaya zaidi ya 80 lakini kilichoshangaza baada ya kuondoka CCM, alifuatana na genge la wachumia tumbo wachache wasiozidi kumi ambao wengine wameanza kurudi CCM. Hii ilikuwa ni ishara halisia kuwa Lowassa ni msanii.

Mama Wema na yeye ameingia CHADEMA kwa kutumia gia kama ya Lowassa ambapo wakati akiongea na vyombo vya habari alisema ana watu zaidi ya 5,000 nyuma yake huku familia yake yenye watu zaidi ya 70 wamemwambia wanajiandaa kuingia CHADEMA.

Tunaelewa Lowassa aliingia na gia hii ili aweze kupewa nafasi ya kugombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya CHADEMA.

Swali la kujiuliza, Mama Wema ameingia na gia kama ya Lowassa ili yeye na mwanae wapate nini CHADEMA? Ubunge wa Viti Maalum? Mawakili wa bure kutoka CHADEMA?

Kinachoshangaza zaidi, kuna baadhi ya vijana wa CHADEMA katika mkutano huo walikuwa wanamshangilia wakati akielezea uwongo wake.

Mwl. Nyerere aliwahi kusema, ‘’Ukiona mtu anakwambia jambo la kipumbavu na yeye mwenyewe anajua kuwa unajua ni la kipumbavu..ukilikubali ujue atakudharau’’.
 
Lowassa aliingia CHADEMA kwa usanii wa kuja na wabunge 50 wa CCM, wenyeviti wa mikoa wa CCM zaidi ya 22, Wenyeviti wa wilaya zaidi ya 80 na wakuu wa wilaya zaidi ya 80 lakini kilichoshangaza baada ya kuondoka CCM, alifuatana na genge la wachumia tumbo wachache wasiozidi kumi ambao wengine wameanza kurudi CCM. Hii ilikuwa ni ishara halisia kuwa Lowassa ni msanii.

Mama Wema na yeye ameingia CHADEMA kwa kutumia gia kama ya Lowassa ambapo wakati akiongea na vyombo vya habari alisema ana watu zaidi ya 5,000 nyuma yake huku familia yake yenye watu zaidi ya 70 wamemwambia wanajiandaa kuingia CHADEMA.

Tunaelewa Lowassa aliingia na gia hii ili aweze kupewa nafasi ya kugombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya CHADEMA.

Swali la kujiuliza, Mama Wema ameingia na gia kama ya Lowassa ili yeye na mwanae wapate nini CHADEMA?

Kinachoshangaza zaidi, kuna baadhi ya vijana wa CHADEMA katika mkutano huo walikuwa wanamshangilia wakati akielezea uwongo wake.

Mwl. Nyerere aliwahi kusema, ‘’Ukiona mtu anakwambia jambo la kipumbavu na yeye mwenyewe anajua kuwa unajua ni la kipumbavu..ukilikubali ujue atakudharau’’.
Achana na longolongo....... Lete ideas tunakuaje nchi ya viwanda? Andika aya kama 4 hivi. Utatusaidia sana kama serikali. Otherwise na wewe tukupuuze
 
Ukisikia uelewa mdogo na hafifu ndio huu! Wenye uelewa hafifu wanadhani kuwa nyuma ya mtu ni hadi uchukue kadi kama yeye na kuhamia alikohamia huku wakisahau what matters nini una-support ndani ya nafsi yako!!

Tumchukulie Emmanuel Nchimbi kwa mfano! Ni mjinga tu ndie atakayeamini kwamba Nchimbi alimpigia kura JPM na sio Lowassa hata kama bado ana kadi ya CCM!!!

Wenye uelewa mpana wanafahamu who's Wema Sepetu! Binafsi ingawaje sio shabiki wa Wema lakini wakati mwingine huwa siachi kujiuliza power ya Wema inasababishwa na nini hasa!! Manake kama hoja ni uigizaji; hata ukuliza filamu yake ya mwisho kaitoa lini wala hakuna atakayekupa jibu!!!

Kwa upande mwingine, watu wa digital world wanafahamu the power of social network and exponential shift from real/physical to cyber world! Na ni kutokana na hii shift ndio maana hivi sasa duniani kuna online political platforms similar to Salesforce and the like ambazo zipo kwa ajili ya kujenga political base.

Mtu kama Wema hivi sasa ana 2.6 Million Instagram Followers!! Ni Wema huyu huyu mwaka juzi; ile tu kusema anam-support Davido na sio Diamond; hapo hapo mashabiki wake wote wakahamia kwa Davido na kumtosa Mtanzania mwenzao na Davido akamdondosha Diamond.

Mange Kimambi na ujeuri wake wote mbele ya Wema anakuwa kama msichana wa shule!!!

Ukiona hadi mawaziri na wabunge wa CCM wanaparuana kwa ajili ya Wema basi ni mjinga tu ndie anaweza kumpuuza!!!

Ni Wema huyu huyu ambae wakati mwingine huwa anawawakia kweli kweli mashabiki wake lakini wapi... ndo kwanza wanazidi kumganda utadhani ruba!!!

The best thing kwa Wema in politics ni kwamba aina ya mashabiki wake hawaelekei kuwa ni wafuasi au die hard fans wa siasa!! Kutokana na hilo, ni rahisi sana kuwa-influence wafuate anachokifuata yeye!! Hawa ni wale ambao wapo tayari ku-sacrifice furaha zao for the sake of Wema's happiness!!

But on top of that, mashabiki wengi wa Wema ni wasichana!! Kwa kawaida wasichana sio mashabiki wakubwa wa siasa na wala sio wapiga kura!! Lakini kwavile wapo very loyal kwa Wema; ni rahisi sana kumfuata kwa ajili tu ya kuonesha support yao kwake!!

Narudia... kumfuata mtu sio lazima wachukue kadi za CHADEMA!!! Hii sio aina ya mashabiki wa Wema! Bali ni mashabiki ambao akiwaambia "...tufanye ABC....!" wanafanya bila kujiuliza mara mbili!!!
 
Achana na longolongo....... Lete ideas tunakuaje nchi ya viwanda? Andika aya kama 4 hivi. Utatusaidia sana kama serikali. Otherwise na wewe tukupuuze
Mambo ya viwanda utapata kwenye jukwaa la Biashara na Uchumi. Hili ni jukwaa la siasa.

Kama unataka mambo ya viwanda, ingia hapa;

LINK Biashara, Uchumi na Ujasiriamali

By the way, Kama ungekuwa unanipuuza wala usingepoteza muda wako kusoma na kutoa komenti.
 
Ukisikia uelewa mdogo ndio huu! Wenye uelewa hafisfu wanadhani kuwa nyuma ya mtu ni hadi uchukue kadi kama yeye na kuhamia alikohamia huku wakisahau what matters nini una-support ndani ya nafsi yako!

Tumchukulie Emmanuel Nchimbi kwa mfano! Ni mjinga tu ndie atakayeamini kwamba Nchimbi alimpigia kura JPM na sio Lowassa hata kama bado ana kadi ya CCM!!!

Umemjibu vizuri sana.
 
Achana na longolongo....... Lete ideas tunakuaje nchi ya viwanda? Andika aya kama 4 hivi. Utatusaidia sana kama serikali. Otherwise na wewe tukupuuze

Ni usanii wa hali ya juu, ulaya na marekani wanaita 'political spinning' yaani kwa lugha ya kifasaha "watu wa kuzungusha maneno"

MsemaUkweli, na wewe ni wakuzungusha uhalisi wa ukweli, unaongelea uroho wa mtoto, baba kaficha chungu cha mchuzi uvunguni. And that's a compliment !

Aibu ! Aibu!
 
Kwani wewe thread yangu inakuwasha nini? Si uniachie mimi mwenyewe!

Mambo ya kwenye thread yangu yanakuuma nini?
Kwa hiyo huu uzi umeandika ili usisomwe? Acha kuweweseka jombaa!! Ngoma si yako kibwebwe cha nini? Au ndo tuamini mnaweweseka na Wema kujiunga Chadema?
Kwa lugha fasaha hicho unachokifanya kinaitwa Unafki
 
Ukisikia uelewa mdogo ndio huu! Wenye uelewa hafisfu wanadhani kuwa nyuma ya mtu ni hadi uchukue kadi kama yeye na kuhamia alikohamia huku wakisahau what matters nini una-support ndani ya nafsi yako!

Tumchukulie Emmanuel Nchimbi kwa mfano! Ni mjinga tu ndie atakayeamini kwamba Nchimbi alimpigia kura JPM na sio Lowassa hata kama bado ana kadi ya CCM!!!
Kwanza lazima uelewe kura ni siri ya mtu. Huwezi kuanza kuhesabu kura kwa kutumia hisia. Ni Chimbi pekee anayejua kura yake alimpigia nani.

Pili, Nani amekuambia kama kuwa nyuma ya mtu lazima uchukue kadi ya chama.

Kwa hiyo unakubali kuwa Mama Wema ana kundi la watu 5,000 litamfata CHADEMA?
 
Kwanza lazima uelewe kuwa ni siri ya mtu. Huwezi kuanza kuhesabu kura kwa kutumia hisia.

Pili, Nani amekuambia kama kuwa nyuma ya mtu lazima uchukue fomu
Ni mjinga tu asiyeelewa impact yake!Kuna watu ambao hata siasa hawafatilii,wao wanamchukulia wema kama role model wao,wata mfuata tu huko aliko!Ukiacha mbwembwe,ukatumia akili then utaelewa hoja hii!
 
Mambo ya viwanda utapata kwenye jukwaa la Biashara na Uchumi. Hili ni jukwaa la siasa.

Kama unataka mambo ya viwanda, ingia hapa;

LINK Biashara, Uchumi na Ujasiriamali

By the way, Kama ungekuwa unanipuuza wala usingepoteza muda wako kusoma na kutoa komenti.
Well kwahiyo umepanic Wema kukimbia chama chenu? Kama hawana lolote ni kwa nini usiwapuuze tu?

Au unadhani jukwaa hili ni la porojo? Hebu nenda wewe Instagram funguwa page tuje tukukaguwe utapata wafuasi wangapi na Wema ana wafuasi wangapi.

Hilo lichama lenu mngekuwa na akili timamu JK angebakia kuwa mwenyekiti na huyu mungu wetu abaki tu kuwa mfalme lakini tatizo hamna maono, mpuuzi mmoja tu ambaye majina na elimu yake ni mashaka matupu anawagharimu na bado mnakenuwa meno tu jinga kabisa wewe.
 
Lowassa aliingia CHADEMA kwa usanii wa kuja na wabunge 50 wa CCM, wenyeviti wa mikoa wa CCM zaidi ya 22, Wenyeviti wa wilaya zaidi ya 80 na wakuu wa wilaya zaidi ya 80 lakini kilichoshangaza baada ya kuondoka CCM, alifuatana na genge la wachumia tumbo wachache wasiozidi kumi ambao wengine wameanza kurudi CCM. Hii ilikuwa ni ishara halisia kuwa Lowassa ni msanii.

Mama Wema na yeye ameingia CHADEMA kwa kutumia gia kama ya Lowassa ambapo wakati akiongea na vyombo vya habari alisema ana watu zaidi ya 5,000 nyuma yake huku familia yake yenye watu zaidi ya 70 wamemwambia wanajiandaa kuingia CHADEMA.

Tunaelewa Lowassa aliingia na gia hii ili aweze kupewa nafasi ya kugombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya CHADEMA.

Swali la kujiuliza, Mama Wema ameingia na gia kama ya Lowassa ili yeye na mwanae wapate nini CHADEMA?

Kinachoshangaza zaidi, kuna baadhi ya vijana wa CHADEMA katika mkutano huo walikuwa wanamshangilia wakati akielezea uwongo wake.

Mwl. Nyerere aliwahi kusema, ‘’Ukiona mtu anakwambia jambo la kipumbavu na yeye mwenyewe anajua kuwa unajua ni la kipumbavu..ukilikubali ujue atakudharau’’.
Tokea lini CCM wakaitakia mema CDM? akunwe binti ndani uanze kulia wewe jirani aise kuwa CCM lazima uwe na akili za kichatochato
 
Back
Top Bottom