OgwaluMapesa
JF-Expert Member
- May 24, 2008
- 10,942
- 437
Neno "ningejua" siku zote huja mwisho wa safari katika kipindi cha majuto kwani walisema majuto ni mjukuu.
Nayasema hayo kutokana na hali ya majuto aliyonayo mke wa waziri mkuu Mama Tunu Pinda ambaye anajuta kuwasikiliza Meya wa jiji la Dar es Salaam Didas Masaburi pamoja na mkewe Janet Masaburi waliomshinikiza mumewe Waziri mkuu, Mizengo Pinda agombee urais kumbe walikuwa na malengo na maslahi yao binafsi.
Mama Pinda aliyafunguka waziwazi kwenye msiba wa Baba yake ambapo aliwaeleza marafiki zake (Mama Pinda) wa karibu sana kuwa aliingizwa mjini shule kwa kusikiliza ushauri wa Masaburi wa kumtaka Waziri mkuu Pinda agombee urais ili wajinufaishe na pesa za bure bure wakati wakijua fika Waziri mkuu Pinda hawezi kuwa Rais wa nchi.
Mama Pinda aliwaeleza marafiki zake hao kuwa mara baada ya kuwakubalia na kuanza kuwapatia pesa hawakuwa wakizitumia kwa ajili ya kampeni bali waliishia kujitajirisha huku wakijipigia kampeni wao wenyewe kwenye nafasi wanazo zitarajia kutanga nia na kugombea.
Mama Pinda alibainisha jinsi alivyoingizwa mkenge huo ambao umepelekea mpaka Mama Masaburi kujenga nyumba ya kifahari huko Tabata kinyerezi.
"Huyo Janet (Mama Masaburi) amekarabati nyumba yake ya kifahari huko kinyerezi kwa hela za mume wangu za kampeni" alisema Mama Pinda mbele ya mashosti zake hao pale msibani.
Mpaka dakika hii ninavyoandika uzi huu Mama Pinda alihaidi kwenda kumshauri mumewe waziri mkuu Pinda kuachana na mpango wa kumtumia Masaburi kama kampeni meneja wa urais wa mumewe na akishindwa kufanya hivyo basi aachane kabisa na nia yake ya kutaka kumrithi Rais Kikwete pale ikulu mwaka huu.
Mashosti hao walimweleza Mama Pinda juu ya tambo za Mama Masaburi juu ya maisha mazuri waliyonayo sasa kipindi ambacho wao ndio makampeni meneja wa Pinda.
Ikumbukwe ya kuwa Pinda amekuwa akimpa Masaburi kiasi cha Tsh. milioni mia tano kwa mwezi kwa ajili ya kumfanyia kampeni za urais, pesa ambazo zimeishia mifukoni mwa wajanja hao akina Masaburi walioamua kujitajirisha na kujifanyia kampeni zao binafsi.
Kweli mjini shule na siku zote wajinga ndio waliwao.
Nayasema hayo kutokana na hali ya majuto aliyonayo mke wa waziri mkuu Mama Tunu Pinda ambaye anajuta kuwasikiliza Meya wa jiji la Dar es Salaam Didas Masaburi pamoja na mkewe Janet Masaburi waliomshinikiza mumewe Waziri mkuu, Mizengo Pinda agombee urais kumbe walikuwa na malengo na maslahi yao binafsi.
Mama Pinda aliyafunguka waziwazi kwenye msiba wa Baba yake ambapo aliwaeleza marafiki zake (Mama Pinda) wa karibu sana kuwa aliingizwa mjini shule kwa kusikiliza ushauri wa Masaburi wa kumtaka Waziri mkuu Pinda agombee urais ili wajinufaishe na pesa za bure bure wakati wakijua fika Waziri mkuu Pinda hawezi kuwa Rais wa nchi.
Mama Pinda aliwaeleza marafiki zake hao kuwa mara baada ya kuwakubalia na kuanza kuwapatia pesa hawakuwa wakizitumia kwa ajili ya kampeni bali waliishia kujitajirisha huku wakijipigia kampeni wao wenyewe kwenye nafasi wanazo zitarajia kutanga nia na kugombea.
Mama Pinda alibainisha jinsi alivyoingizwa mkenge huo ambao umepelekea mpaka Mama Masaburi kujenga nyumba ya kifahari huko Tabata kinyerezi.
"Huyo Janet (Mama Masaburi) amekarabati nyumba yake ya kifahari huko kinyerezi kwa hela za mume wangu za kampeni" alisema Mama Pinda mbele ya mashosti zake hao pale msibani.
Mpaka dakika hii ninavyoandika uzi huu Mama Pinda alihaidi kwenda kumshauri mumewe waziri mkuu Pinda kuachana na mpango wa kumtumia Masaburi kama kampeni meneja wa urais wa mumewe na akishindwa kufanya hivyo basi aachane kabisa na nia yake ya kutaka kumrithi Rais Kikwete pale ikulu mwaka huu.
Mashosti hao walimweleza Mama Pinda juu ya tambo za Mama Masaburi juu ya maisha mazuri waliyonayo sasa kipindi ambacho wao ndio makampeni meneja wa Pinda.
Ikumbukwe ya kuwa Pinda amekuwa akimpa Masaburi kiasi cha Tsh. milioni mia tano kwa mwezi kwa ajili ya kumfanyia kampeni za urais, pesa ambazo zimeishia mifukoni mwa wajanja hao akina Masaburi walioamua kujitajirisha na kujifanyia kampeni zao binafsi.
Kweli mjini shule na siku zote wajinga ndio waliwao.