Queen V
JF-Expert Member
- Jan 19, 2012
- 776
- 1,330
Jamani mji haukosi issue huu..
Katika episode latest ya shoo ya Miss Tanzania 2006, Mlezi wa Wana Originali (akina Shishi wanacopy tu), Wema Abraham Sepetu iitwayo Cook with Wema Sepetu mgeni alikuwa Mama wa Steve Kanumba.
Katika Mahojiano kati ya Wema na Mama Kanumba wakiwa wanapika ndizi, mama Kanumba alisema mwanae aliuawa.
Wema akauliza swali ambalo limempatia lawama kibao. Swali lilikuwa “nani alimuua? Leo nataka ufunguke mama”.
Mama naye hakuwa na kukopesha wala kupindisha akamtaja Lulu kwa jina lake la Serikali - Elizabeth Michael.
Katika inayoonesha ni kuendeleza chokochoko, Wema akaenda kupost clip ambapo Mama Kanumba anasema yeye ndo binti pekee aliyewahi kupelekewa na mwanaye huku akitamba kwamba hajawahi kuchukiwa na mkwe hata siku moja. Yani waja wengine mnaweza kumchukia ila anashukuru alhamdulillah hajawahi kuchukiwa ukweni.
Hii imechukuliwa kama dongo kwa Lulu ambaye maneno mtaani yanadai ndoa yake imepigwa breki na wakwe ambao hawataki kumsikia kwa tuhuma za kuwa mchawi.
Kwakweli jamii ya Instagram haijafurahishwa kabisa na Wema. Amechambwa kushoto, kulia na katikati.
Wananzengo walivyo wachokozi wakaenda kwenye comments za post za Lulu na kumdokeza yaliyojiri.
Majibu ya Lulu ni kama ifuatavyo:
Inaelezwa kuwa Lulu ameshamblock “shosti” wake huyo ambaye juzi kati tu walikuwa wanaitana “babe” kwenye kipindi hicho hicho cha Wema.
Taarifa zisizo rasmi zinadai kamwe Lulu na Wema hawawezi kupatana kwani wameshapita sehemu hizo hizo ikiwemo kwa Kanumba, Mr. Blue, Idris na Majizo.
Katika episode latest ya shoo ya Miss Tanzania 2006, Mlezi wa Wana Originali (akina Shishi wanacopy tu), Wema Abraham Sepetu iitwayo Cook with Wema Sepetu mgeni alikuwa Mama wa Steve Kanumba.
Katika Mahojiano kati ya Wema na Mama Kanumba wakiwa wanapika ndizi, mama Kanumba alisema mwanae aliuawa.
Wema akauliza swali ambalo limempatia lawama kibao. Swali lilikuwa “nani alimuua? Leo nataka ufunguke mama”.
Mama naye hakuwa na kukopesha wala kupindisha akamtaja Lulu kwa jina lake la Serikali - Elizabeth Michael.
Katika inayoonesha ni kuendeleza chokochoko, Wema akaenda kupost clip ambapo Mama Kanumba anasema yeye ndo binti pekee aliyewahi kupelekewa na mwanaye huku akitamba kwamba hajawahi kuchukiwa na mkwe hata siku moja. Yani waja wengine mnaweza kumchukia ila anashukuru alhamdulillah hajawahi kuchukiwa ukweni.
Hii imechukuliwa kama dongo kwa Lulu ambaye maneno mtaani yanadai ndoa yake imepigwa breki na wakwe ambao hawataki kumsikia kwa tuhuma za kuwa mchawi.
Kwakweli jamii ya Instagram haijafurahishwa kabisa na Wema. Amechambwa kushoto, kulia na katikati.
Wananzengo walivyo wachokozi wakaenda kwenye comments za post za Lulu na kumdokeza yaliyojiri.
Majibu ya Lulu ni kama ifuatavyo:
Inaelezwa kuwa Lulu ameshamblock “shosti” wake huyo ambaye juzi kati tu walikuwa wanaitana “babe” kwenye kipindi hicho hicho cha Wema.
Taarifa zisizo rasmi zinadai kamwe Lulu na Wema hawawezi kupatana kwani wameshapita sehemu hizo hizo ikiwemo kwa Kanumba, Mr. Blue, Idris na Majizo.