Mateso
JF-Expert Member
- Aug 6, 2008
- 259
- 19
Ni muda mrefu tumekuwa tukimsikia Mheshimiwa Makufuli akiwataka wavuvi wanaotumia nyavu ndondogo wengine wanaita korokoro wazisalimishe au wakikamatwa watachukuliwa hatua za kisheria. Kimsingi wavuvi hawa wamekuwa wakijipatia riziki zao za kila siku kwa nyavu hizo ndogondogo. Sasa wengi wamesalimisha nyavu zao na hawana namna ya kujipatia mkate wao wa kila siku pengine watoto wanaweza wakashindwa kwenda shule hapo baadaye. SASA kwa nini Makufuli asiwajibike kuwatafutia miokpo ya kuwanunulia nyavu halali wale wanaosalimisha nyavu zao kwa hiyari yao ili awashawishi na wengine kusalimisha zao? Nasema hivyo kwa sababu kama mtu anajua akisalimisha nyavu zake watoto watakufa njaa hatakuwa tayari kufanya hivyo. WADAU MNASEMAJE?