Makonda amtumia Mwamposa kupata umaarufu kwa kisingizio cha Salamu za Rais Samia , ni mbinu duni sana

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,798
218,442
Naamini sana maombi ya Mwamposa , lakini nakataa Mtume huyu kujaribiwa kama vile Yesu alivyojaribiwa na Shetani .

Makonda si msemaji wa Ikulu , hawezi kuleta uongo kwamba kabeba salamu za Rais kwenye Vuka na chako , hizi ni siasa duni sana .

Nikiwa kama muamini Mungu na muamini matendo Makuu ya Mungu napinga wanasiasa duni wenye makando kando kujichomeka kwenye nyumba za ibada .

Natoa wito kwa Viongozi wa dini na Manabii kuepuka kujivunjia heshima kwa kujaribu kuwakumbatia viongozi wahuni kwa style ya mchongo , Mungu hataniwi .

Naomba kuwasilisha .
 
Wapo ma nabii wa uongo

Sent from my Infinix X688B using JamiiForums mobile app
Maana yake hakuna nabii kuna matapeli tu

Yaan Bora nilipata kufaulu bila kwenda kwenye makanisa ya mtu namaliza chuo nasaga soli naambiwa nenda kwenye maombi nikasema wapi hunipeleki Mimi nimekaa kazi hii hapa nimeula ingekua nimeenda huko wangenipa Maiki nitoe ushuhuda pumbavu matapeli watawatapeli mazombi tu sio wenye akili timamu na wanaojielewa
 
Naamini sana maombi ya Mwamposa , lakini nakataa Mtume huyu kujaribiwa kama vile Yesu alivyojaribiwa na Shetani .

Makonda si msemaji wa Ikulu , hawezi kuleta uongo kwamba kabeba salamu za Rais kwenye Vuka na chako , hizi ni siasa duni sana .

Nikiwa kama muamini Mungu na muamini matendo Makuu ya Mungu napinga wanasiasa duni wenye makando kando kujichomeka kwenye nyumba za ibada .

Natoa wito kwa Viongozi wa dini na Manabii kuepuka kujivunjia heshima kwa kujaribu kuwakumbatia viongozi wahuni kwa style ya mchongo , Mungu hataniwi .

Naomba kuwasilisha .
hahaaaa utakufa na presha unamuwaza makonda hujazaa mimba yake
 
Bahati mbaya zaidi kwako,,,watumishi wa Mungu wa kweli ndio wameitiwa kuwaendea waovu.

Wanafunzi wa Yesu walimkasirikia kwa kwenda nyumbani kwa Zakayo mtoza ushuru na mwizi.

Yesu alilijua hilo lakini alitimiza kusudi lake.

Mkuu hiyo hoja ya watumishi kuwatenga wenye makandokando inakufia hapa
 
Back
Top Bottom