makocha wa timu za taifa wanatak kujulikana au wanapowaacha nyota world cup?

bona

JF-Expert Member
Nov 6, 2009
3,798
1,435
wakati tukiwa ktk countdown ya mechi ya kwanza kuanza kombe la dunia, kuna kitu bado nna hasira nacho kwa tabia ya makocha na wamekua wakiigana cjui kwa kutaka umaarufu au la pale wanapowaacha wachezaji ambao kila mtu anaona ni kama lazima walitakiwa wawepo, chini ni mifano michache

1. ronaldinho
kitendo cha dunga kumuacha dinho, burudani imepungua sana south, ivi kati ya dinho na grafite, gilberto walioenda nani bora?

2. kevin kuranyi
kitendo cha leow kumuacha kuranyi ktk kikosi cha ujerumani wakati alikua top score bundliga kinashangaza, forward walioenda jumla ya magoli yao hayafikii aliofunga kuranyi.

3. benny mc carhty
kitendo cha perreira kumuacha maccarthy kikosi cha south kinashangaza, ni forward with plenty of experince with big games, forward waliokuwepo hata kwa sasa kama wako kwenye form hawana experinece ya big game.

4. cambiasso, zanneti
kitendo cha maradona kuwaacha ktk kikosi cha argentina wakati ndio waliiiwezesha inter kushinda champions league akapelekwa mtu kama veron, parlemo inaingia akilini kweli.

5. nasri, viera na benzema
kitendo cha kocha wa ufaransa kuwaacha hawa vijana kwa timu inayochechemea kama ufaransa ni dhihaki kubwa tena bila kuwapigia simu.

6. theo walcot
hivi theo walcot na heskey kweli kuna ulinganifu?

nahisi kama makocha wanapenda sifa tu ilimradi asikike kua fulani haendi world cup? inasikitisha sana makocha wanaviburi na wanapewa madaraka makubwa hata kama nchi nzima au dunia zinaona si sawa!
 
Back
Top Bottom