Makinikia: Nilisema..Na ninasema!

Adrian Stepp

R I P
Joined
Jul 1, 2011
Posts
2,764
Reaction score
2,600
Wakuu,

Tarehe 26 August niliandika niliweka bandiko kuhusu sakata la makinikia:


Kinacho endelea hivi sasa juu ya "Sintofahamu" kati ya wawekezaji na serikali kila mfuatiliaji anakijua..

Nitoe rai kwa serikali na watunga Sera kuamka na kuanza upya ili huko mbeleni tuepukane na kadhia hii ya "Mtu mzima kuvuliwa taulo" .

Kuendelea kujifariji kipuuzi kwamba Tanzania ni taifa changa na kelele za wanasiasa kutumia umasikini kama sifa ..zama hizo zimepitwa na wakati!

Wakati ni sasa! Nilisema, Ninasema na Nitasema kwamba kuanza upya si ujinga!

Jumapili njema!
 
Hebu justify kuachana na Trilion 425, ambayo ni bajeti ya nchi kwa miaka 14 bila msaada wa senti za wahisani!. Ningekuona una hoja ya msingi ungesema tuwapeleke ACACIA mahakamani kwa wizi wote wa madini walioufanya sababu ushahidi wa kisayansi tunao!!
 
Tanzania yetu siyo tajiri kihivyo kama mnavyoamini, ni kweli tuna Rasilimali za kutosha lkn wengine wanazo pia, hivyo tufute hilo kwamba sisi ndiyo Matajiri Duniani huwo siyo ukweli, ukweli ni kwamba tuna Rasilimali za kututosha kuishi vizuri kama tukiwa makini, lkn hatuna upekee wowote ule!

Haya mambo ndiyo yanayofanya watu wawe na matarajio ambayo hayapo, semeni ukweli na siyo propaganda kwamba sijui nchi yetu imebarikiwa na Rasilimali klk zote, hiyo ni bullshit, kwani wengine wanazo pia!
 
Huu ndio ushauri wa maana unaolisaidia Taifa
sio wale Vibendera na lichama lao la Vibendera kutwa kuomba mabaya tu kwa taifa!

Ndio maana ikaletwa sheria na Wazungu kupata kiwewe kikubwa kwenya majadiliano.

Tuzidi kumuunga mkono mh Rais wetu
huyu ana nia njema kwa Taifa
 
Aliye kuambia Matajiri kuliko wote nani!

Utajiri wa nchi ni Rasilimali zake
Tunathubutu kusema tena kwa kifua mbele Sisi matajiri
 
Mkuu nawe unalijua hili?
 
Adrian Stepp


Mkuu umenena japo bandiko lako limekua abstract Sana kwenye recommendation.

Kwa ufananuzi tu ni kwamba:-.
Utawala uliopo unajinasibu kua ndio umeshiba uzalendo WA kipimo cha Ghorofa.

Lakini kila wakiita press wanatudanganya kwa uongo wa ghorofa la Burji khalifa.

Wanatembelea kiki, vitisho na wasiojulikana.

Sasa sijui Kama tumeanza upya ama ni style mpya ya nitoke vipi!!?
 
I didn’t expect sense coming from, mmmmm!
 


Hebu justify kuachana na Trilion 425, ambayo ni bajeti ya nchi kwa miaka 14 bila msaada wa senti za wahisani!. Ningekuona una hoja ya msingi ungesema tuwapelekeACACIA mahakamani kwa wizi wote wa madini walioufanya sababu ushahidi wakisayansi tunao!! By Gamba la Nyoka
 
Basi wawe wanasema ukweli kama jamani tumepigwa tuanze upya! sio kukaa kutupigia kelele zisizo Na maana eti tumsifie jpm.....Na kila anayekosoa sio mzalendo!
Well said
 
Kama kuna anayepinga 50-50 aje atuambie inatakiwe iwe ngapi kwa ngapi?
 
Baki hapo kwenye Gesi Je hautupigwi? Mitambo ya kuangalia nini kinaendelea kwenye Gesi iko Uingereza Ulinzi wanafanya wenyewe
 
Sina uhakika kama hata sisi wenyewe kama taifa tuna confidence na ushahidi wetu. Nadhani ndiyo maana tunasita kwenda mahakamani kuhofia kuvuliwa nguo.
 

Nikiangalia umasikini uliopo congo DRC na wana madini karibu aina zote duniani tena kwa wingi, siwezi kuamini kwamba eti sisi ndo matajiri, hayo ni maneno ya kisiasa tu kwa ajili ya kura.
 
Hiyo hoja yako ya kuipeleka serikali mahakamani iandikie bandiko lako..kwanini unamlazimisha mtoa mada afuate unacho taka?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…