Mangandula
Senior Member
- Nov 30, 2011
- 184
- 37
Nipo ndani ya basi natoka mbeya naingia makambako standi nakaribishwa na madimbwi! Hivi jamani hivi si vitega uchumi vinavyoingiza fedha kila iitwapo leo? Je viongozi hamuoni kama kuna umuhimu wa kuikarabati hii standi ili mpate malipo ya haki? Mbunge uko wapi? Diwani wa eneo hilo uko wapi? Hakika hii ni kero kwa walipa kodi na abilia kwa ujumla. Nimeambiwa na wenyeji kuwa kila wakipiga kelele au kutoa maoni kuhusu hii standi wanapata misukosuko! Mara wataambiwa wao ni wapinzani, pia nasikia waandishi wa habari wengi wameenda eneo la tukio na kuhoji lakini pindi wanapoondoka tu cha moto lazima wakipate. Leo mjaribu kuwasumbua muone! Badala ya kushughulikia matatizo yanayowakabili wananchi mnawanyanyasa wapiga kura wenu! Shughulikieni tatizo la maji, barabara na watendaji wanaotafuna fedha za maendeleo.