Sir robby
JF-Expert Member
- Jun 22, 2022
- 2,393
- 4,083
Wadau nawasalimu,
Pamoja na Rais kusema Mzee Makamba ulimi uliteleza binafsi siamini hivyo, kwani huyu Mzee kabla ya kuyazungumza hayo ndani ya kikao alipokuwa nje ya ukumbi aliropoka mambo mengi ambayo kwa umri wake na nyadhifa alizopitia hakustahili kuyasema.
Mzee alionekana mwenye jazba labda kwa kuwa swali aliloulizwa lilimhusu mtoto wake January la kukatika katika kwa umeme. Kwa hili la kusema watu wazuri hawafu binafsi naamini alilipanga muda mrefu. Wenye akili kubwa tunajua kwanini kalisema na alimlenga/kuwalenga kina nani.
Ila tunamwambia Mzee Yusuf Makamba ya kuwa, Mungu hadhihakiwi, yeye pia ni mavumbi hataishi milele pamoja na hao wazuri wakina Kinana na Kikwete, ipo siku mavumbini atarudi.
Pamoja na Rais kusema Mzee Makamba ulimi uliteleza binafsi siamini hivyo, kwani huyu Mzee kabla ya kuyazungumza hayo ndani ya kikao alipokuwa nje ya ukumbi aliropoka mambo mengi ambayo kwa umri wake na nyadhifa alizopitia hakustahili kuyasema.
Mzee alionekana mwenye jazba labda kwa kuwa swali aliloulizwa lilimhusu mtoto wake January la kukatika katika kwa umeme. Kwa hili la kusema watu wazuri hawafu binafsi naamini alilipanga muda mrefu. Wenye akili kubwa tunajua kwanini kalisema na alimlenga/kuwalenga kina nani.
Ila tunamwambia Mzee Yusuf Makamba ya kuwa, Mungu hadhihakiwi, yeye pia ni mavumbi hataishi milele pamoja na hao wazuri wakina Kinana na Kikwete, ipo siku mavumbini atarudi.