Kibo10
JF-Expert Member
- Aug 20, 2013
- 11,278
- 8,868
Watu watatu wanaosadikiwa kuwa majambazi wameuawa kwa kupigwa na kuchomwa moto na wananchi wenye hasira kali baada ya kudaiwa kuvamia duka la bidhaa mbalimbali eneo la Tabata Matumbi jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuiba.
Inadaiwa kwamba baada ya kumjeruhi muuza duka na kushindwa kutumia bastola waliyokuwa nayo majambazi hao wamejikuta wakikamatwa na kuadhibiwa na wananchi hao.
ITV ikiwa katika eneo la tukio imeshuhudia majambazi hao wakipigwa na kuchomwa moto kabla ya polisi kufika na kuchukua miili ya majambazi hao na kuipekela katika hospitali ya taifa ya Muhimbili ikiwa imekwishaungua vibaya.
Inadaiwa kwamba baada ya kumjeruhi muuza duka na kushindwa kutumia bastola waliyokuwa nayo majambazi hao wamejikuta wakikamatwa na kuadhibiwa na wananchi hao.
ITV ikiwa katika eneo la tukio imeshuhudia majambazi hao wakipigwa na kuchomwa moto kabla ya polisi kufika na kuchukua miili ya majambazi hao na kuipekela katika hospitali ya taifa ya Muhimbili ikiwa imekwishaungua vibaya.