Utata huo ulizuka jana maeneo ya Tandale Magharibi, baada ya wanaume wawili mmoja aitwae Abdul na mwingine Salum kugombania maiti ya mwanamke mmoja aitwae Tausi Hassan [36] kila mmoja akidai alikuwa mkewe wa ndoa akitaka kwenda kuuzika.
Zogo hilo lilizuka baada ya Tausi pamoja na mwanae aitwae Faim Salum kufariki dunia baada ya marehemu na mwanae wakiwa kwenye bajaji kugongwa na gari la taka eneo la Magomeni Mapipa.
Inadaiwa na ndugu wa karibu wa mume wa kwanza wa marehemu kuwa, wakiwa nyumbani kwa mume wa marehemu wakijitayarisha na taratibu za mazishi walijitokeza wanawake wapatao watano wenye asili ya kiarabu wakidai wapewe miili yote miwili Tausi na mwanae waende kuizika.
Katika kitu ambacho hakuna mtu ambaye alitegemea mahali pale wakinamama hao walitoa cheti cha ndoa kinachoonyesha Abduli na Tausi walifunga ndoa huko Kariakoo Mtaa wa Jangwani jijini Dar es salaam.
Baada ya zogo kubwa kuzuka ndugu wa marehemu waliamua kuuchukua mwili huo na kwenda kuzika kijijini kwao Tungi Mkoani Morogoro.
Inadaiwa kuwa marehemu alifunga ndoa na wanaume wawili bila mume wake wa kwanza kutambua hilo.
Inadaiwa kuwa kwa mara ya kwanza marehemu alifunga ndoa na Salum Senela mwaka 1998.
Pia mwanzoni mwa mwaka jana marehemu ilidaiwa kafunga tena ndoa na Abdul hapahapa jijini Dar e salaam.
Inadaiwa marehemu alikuwa anaweza kuzimiliki ndoa hizo mbili bila wasiwasi na alikuwa anawapa zamu wanaume hao bila kutambua kinachoendelea.
Jamii na ndugu zake marehemu wamesikitishwa sana na tukio hilo kwa kuwa walikuwa hawafahamu kama alikuwa na waume wawili na ajali hiyo ya gari ndio iliyosababisha yajulikane yote hayo.
Source: Nifahamishe.com
Zogo hilo lilizuka baada ya Tausi pamoja na mwanae aitwae Faim Salum kufariki dunia baada ya marehemu na mwanae wakiwa kwenye bajaji kugongwa na gari la taka eneo la Magomeni Mapipa.
Inadaiwa na ndugu wa karibu wa mume wa kwanza wa marehemu kuwa, wakiwa nyumbani kwa mume wa marehemu wakijitayarisha na taratibu za mazishi walijitokeza wanawake wapatao watano wenye asili ya kiarabu wakidai wapewe miili yote miwili Tausi na mwanae waende kuizika.
Katika kitu ambacho hakuna mtu ambaye alitegemea mahali pale wakinamama hao walitoa cheti cha ndoa kinachoonyesha Abduli na Tausi walifunga ndoa huko Kariakoo Mtaa wa Jangwani jijini Dar es salaam.
Baada ya zogo kubwa kuzuka ndugu wa marehemu waliamua kuuchukua mwili huo na kwenda kuzika kijijini kwao Tungi Mkoani Morogoro.
Inadaiwa kuwa marehemu alifunga ndoa na wanaume wawili bila mume wake wa kwanza kutambua hilo.
Inadaiwa kuwa kwa mara ya kwanza marehemu alifunga ndoa na Salum Senela mwaka 1998.
Pia mwanzoni mwa mwaka jana marehemu ilidaiwa kafunga tena ndoa na Abdul hapahapa jijini Dar e salaam.
Inadaiwa marehemu alikuwa anaweza kuzimiliki ndoa hizo mbili bila wasiwasi na alikuwa anawapa zamu wanaume hao bila kutambua kinachoendelea.
Jamii na ndugu zake marehemu wamesikitishwa sana na tukio hilo kwa kuwa walikuwa hawafahamu kama alikuwa na waume wawili na ajali hiyo ya gari ndio iliyosababisha yajulikane yote hayo.
Source: Nifahamishe.com